Wazee wa Mkoa wa Pwani wamewataka vijana kujitambua, kuzingatia maadili na kuendeleza uzalendo kwa Taifa, wakisisitiza umuhimu wa kuepuka vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani.
Akizungumza leo Desemba 3 mjini Kibaha, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Ushauri Mkoa wa Pwani, John Kirumbi, amesema vijana wanapaswa kuishi kwa maadili waliyofunzwa na wazazi wao na kutanguliza uzalendo katika maisha yao.
Wazee hao wamekutana na waandishi wa habari kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa hotuba yake ya Desemba 2 aliyoitoa kwa wazee wa Dar es Salaam. Kirumbi amesema wao kama wazee wa Pwani wako tayari kusimama imara kulinda amani, umoja na maadili ya Taifa kwa kutumia hekima yao kuwaongoza vijana.
Kirumbi pia amemshukuru Rais Samia kwa kutambua mchango wa wazee kama nguzo ya busara na mshikamano, akisema hatua hiyo imewapa moyo kuendelea kuchangia hekima katika kuimarisha amani na umoja wa Taifa.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
Sanduku la Posta: 30080 Kibaha
Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500
Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500
Barua pepe: barua@pwani.go.tz
Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.