• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Waziri Kairuki awataka Viongozi Pwani Shughulikia Changamoto na kero za walimu.

Posted on: January 10th, 2023

WaziriI wa Nchi,Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Angela Kairuki,amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge pamoja na Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanafuatilia ufundishaji wa walimu ili kuweza kuboresha elimu

Pamoja na hilo lakini pia amewataka viongozi hao kushughulikia changamoto na kero za walimu hususani katika kuwalipa stahiki zao ikiwemo fedha za malimbizo ya mishahara na madeni mbalimba ili waweze kufanya kazi zao kwa umahiri.

Kairuki,ametoa maagizo hayo katika kikao kazi cha mapitio ya tathimini ya utekelezaji wa shughuli za uboreshaji na usimamizi wa elimu kwa mwaka 2022 na mpango wa mwaka 2023 kilichofanyika katika viwanja vya Shirika la Elimu Kibaha.

Katika kikao hicho kilichowakutanisha maafisa mbalimbali wa elimu kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Pwani,Wakurugenzi wa Halmashauri ,maafisa elimu Kata,Wakuu wa Shule pamoja na viongozi wengine kilikuwa na lengo la kukumbushana namna ya kuboresha elimu ya Msingi na Sekondari.

Kairuki, alisema kuwa Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imefanyakazi kubwa katika kuboresha mazingira ya ufundishaji kwa walimu na hata kutatua changamoto nyingine.

Aidha ,Kairuki amemshukuru Rais Samia kwa jitihada hizo maana angeweza kuingia madarakani na kufuta mpango wa elimu bure lakini cha ajabu katika kipindi kifupi cha Novemba 2021 na Desimba 2022 ameendeleza zaidi mpango huo na kuweza kujenga madarasa 23000 .

Kairuki, ameongeza kuwa pamoja nakujenga madarasa hayo lakini bado ameendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kujenga Shule mpya katika Mikoa mbalimbali hapa nchini zikiwemo Shule za Sekondari za wasichana

"Tumeona jinsi ambavyo Rais wetu anavyofanyakazi hususani katika sekta hii ya elimu kwahiyo niwaombe tuendelee kuyasemea mafanikio haya ili kuweza kumtia moyo Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa

Kairuki ,pamoja na mafanikio makubwa yaliyopo lakini bado zipo changamoto mbalimbali ikiwemo watoto wa awali kushindwa kusoma na kuandika ,pamoja na wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza kushindwa kuongea lugha ya kiingereza.

Alisema,sio changamoto hiyo tu lakini kuna sababu za kimila na desturi pamoja na utoro zinazosababisha watoto kushindwa kufikia malengo na kwamba amewataka maafisa hao kubuni mikakati sahihi ya kuthibiti changamoto hizo.

Mbali na kikao hicho lakini pia Kairuki akiwa Mkoani Pwani alitembelea na kukagua Shule ya Sekondari Sofu pamoja iliyopo Mjini Kibaha na kufuruhishwa na ujenzi huo huku akiwataka walimu kusimamia vyema miundombinu ya Shule hizo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge,alisema kuwa tayari Mkoa ulishafanya kikao kama hicho na utekelezaji wake umekwenda vizuri.

Kunenge,alisema kuwa walifanya tathmini na kubaini Mkoa wa Pwani Kuna Mila na desturi na tathmini hiyo ilikuwa pamoja na kuwauliza wanafunzi kama Kuna utaratibu wa masomo wanapofika nyumbani,vitabu na vifaa vingine vya kujisomea.

Aidha, Kunenge amempongeza Rais wa awamu ya Sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya hasa katika kutambua masuala mbalimbali ya elimu yaliyopo Mkoani Pwani.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.