• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Daraja la Wami kuanza kutumika Mwezi Julai

Posted on: May 23rd, 2022

Mradi wa ujenzi wa Daraja jipya la WAMI lenye urefu wa mita 510 na upana wa mita 11.85 linalojengwa umbali wa mita 670 pembeni mwa daraja la zamani linatarajiwa kuanza kutumika Mwezi Julai 2022.

Mradi huo ambao ni moja ya Miradi ya kimkakati inayoendelea kutekelezwa Mkoani Pwani umefikia asilimia 91 huku upande wa barabara unganishi ukiwa umefikia asilimia 79.5.

Hayo yamebainika  Mei 23 wakati Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge alipofanya ziara ya ukaguzi katika baadhi ya miradi ya kimkakati inayoendelea kutekelezwa Mkoani Pwani ambayo yote ipo katika hatua nzuri za uendelezaji na akasema kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo na kuhakikisha kuwa inakamilika ili itoe huduma kwa wananchi.

Kunenge alifafanua kuwa mradi huu ni tunu ya mkoa na Taifa na utagharimu zaidi ya sh. bilioni 75.134 bila VAT na kuwa daraja la WAMI la zamani lilijengwa 1959 na ni kiungo kutoka Chalinze kwenda mikoa ya Kaskazini mwa Tanzania na nchi jirani.

"Daraja lile la zamani halikidhi mahitaji ya magari yanayopita kwa kuwa lilijengwa miaka mingi iliyopita na ni jembamba lenye njia moja, barabara zinazounganisha daraja hili ziko kwenye miinuko mikali na kona mbaya ambapo ajali mbaya na vifo vimekuwa vikitokea mara kwa mara, hivyo hili jipya likikamilika litakuwa Mkombozi." alisema Kunenge.

Aliongeza kuwa baada ya mkandarasi kukamilisha ujenzi huo atafanya ukarabati wa Daraja la zamani ili nalo litoe huduma.

Vilevile Kunenge alikagua Mradi wa barabara ya Kwala -Vigwaza yenye urefu wa kilometa 15.5 inayounganisha barabara Kuu ya Morogoro kupita katika vijiji vya Vigwaza, Mnindi na Kwala ambayo kwa Sasa inajengwa kwa kiwango cha Zege ili kurahishisha shughuli za uchukuzi kati ya bandari na barabara Kuu ya Morogoro.

Awali mwakilishi wa Meneja wa Wakala wa barabara ( TANROADS ) Mkoa wa Pwani Evelyn Mlai alisema kuwa ujenzi wa barabara unganishi utakamilika Novemba mwaka huu ikiwa na urefu wa km. 3.8 inayojengwa kwa kiwango cha lami yenye njia mbili zenye Jumla ya upana wa mita 12 ambazo ni mita 3.5 kwa kila njia ipitishayo magari, mita 2 za bega la lami na mita 0.5 za bega lisilo la lami kila upande.

"Kampuni inayosimamia kazi za ujenzi ni ILSHIN Engineers,& consultant Co. Ltd toka Jamhuri ya Korea Kusini ikishirikiana na Advanced Engineering Solutions Limited ya Tanzania kwa gharama ya sh. bilioni 6.3 bila VAT." alisema Evelyn.

Evelyn alieleza kuwa mkandarasi alianza kazi Oktoba 22 mwaka 2018 na hadi sasa utekelezaji wa kazi umefikia asilimia 79.5 huku katika daraja sehemu ya chini utekelezaji wake umefikia asilimia 100 ikiwemo misingi na nguzo nne na kuta mbili za mwanzo na mwisho wa Daraja.

Nae Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallah alibainisha kuwa daraja hilo litakuwa na uwezo mkubwa katika usafirishaji na kufungua milango ya kimaendeleo na kukuza uchumi wa nchi yetu.

Aliwaambia Wana Bagamoyo Mradi ukikamilika wautumie kama fursa kwao ili kujiongezea tija.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.