• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Halmashauri za <koa wa Pwani zimetakiwa kuhakikisha zinatenga Fedha kwa ajili ya Shughuli za Lishe

Posted on: September 2nd, 2024

Halmashauri katika Mkoa wa Pwani zimetakiwa kuhakikisha kuwa fedha zinazotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za lishe zinatumika kama zilivyopangwa. Aidha, zimetakiwa kutenga fedha kwa ajili ya kununua vibao vya ufuatiliaji wa makuzi ya watoto katika kila kituo cha afya, ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata huduma stahiki za lishe.

Ofisa Lishe wa Mkoa wa Pwani, Mecy Mtaita, akizungumza wakati wa kutoa taarifa ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa kipindi cha Julai 2023 hadi Juni 2024, alibainisha mikakati mbalimbali iliyowekwa ili kufikia malengo ya mkataba huo. Mtaita alieleza kuwa baadhi ya halmashauri zimekuwa zikishindwa kutumia fedha kama ilivyopangwa, hali inayosababisha kudorora kwa utekelezaji wa mipango ya lishe.

"Baadhi ya halmashauri zimefanikiwa kutumia fedha kwa ufanisi, kama vile Halmashauri ya Kibaha Mjini na Kisarawe ambazo zilitumia asilimia 100 ya bajeti zao za lishe. Halmashauri ya Kisarawe ilitumia asilimia 99.5, ambayo pia ni kiwango cha kuridhisha," alisema Mtaita.

Aliongeza kuwa kuna upungufu mkubwa wa vibao vya ufuatiliaji wa makuzi ya watoto, ambapo kibao kimoja kinauzwa kwa kati ya shilingi 250,000 hadi 350,000. Vibao hivi ni muhimu kwani bila ya takwimu sahihi, ni vigumu kufanya maamuzi sahihi katika kupambana na udumavu na ukondefu kwa watoto walio chini ya miaka mitano.

"Ili kufanya tathmini sahihi, ni lazima vituo vya afya viwe na vibao vya kupimia makuzi ya watoto. Kwa sasa tuna asilimia 27 tu ya vibao hivyo, wakati lengo ni kuhakikisha kila kituo kinaweza kufanya tathmini na kuchukua hatua mapema inapohitajika," alisisitiza Mtaita.

Mtaita alieleza kuwa, kuna haja ya kuboresha mipango na bajeti za lishe ili ziweze kuendana na mahitaji halisi ya jamii. Alisisitiza umuhimu wa kuongeza upatikanaji wa huduma za lishe zenye ubora na usawa kwa wote.

Pia, alizitaja changamoto za mkoa, ikiwa ni pamoja na idadi ndogo ya shule zinazotumia unga ulioongezewa virutubishi, pamoja na ukosefu wa vifaa vya kupima iodine (iodine test kits) kwa muda mrefu, jambo ambalo limeathiri uwezo wa kupima uwepo wa madini joto katika chumvi zinazotumiwa na wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, alisisitiza umuhimu wa halmashauri kutoa fedha kwa wakati ili kuhakikisha utekelezaji wa masuala ya lishe unafanikiwa. Alitoa wito kwa viongozi na watendaji wa mkoa kushirikiana kwa karibu ili kuinua maendeleo na uchumi wa mkoa kwa ujumla.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.