• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kamisaa Anne Makinda Azindua Kampeni ya Sensa ya watu na Makazi Pwani.

Posted on: August 4th, 2022

Kamisaa wa Sensa 2022, Anne Makinda ametoa ufafanuzi kwamba ,siku ya sensa Agosti 23 mwaka huu haitakuwa siku ya mapumziko badala yake kila mmoja ataendelea na shughuli za kimaendeleo ,pia amesema , tarehe 23 itakuwa siku maalum ya kuhesabiwa lakini itaendelea taratibu za kuhesabu madodoso Hadi tarehe 28 agost mwaka huu.

Akizungumza katika Kongamano la viongozi wa dini pamoja na kuzindua tangazo la umuhimu wa ushiriki wa sensa alisema ,kila mmoja ana wajibu wa kujisensa mwenyewe kwa kutambua wajibu ni wa kila mmoja .

"Mkoa wa Pwani na wilaya ya Kibaha Nimejifunza Jambo kubwa kujisensa mwenyewe,kilichobaki agost 23 mwaka huu tuweze kujisensa wenyewe ili kupata takwimu sahihi kwani tukifanikiwa Tanzania itakuwa mpya".

“Anne alisema, wamejiandaa vizuri mno kwa kutumia teknolojia ya kisasa (kishkwambi ) kurahisisha uhifadhi wa taarifa tofauti na sensa za miaka iliyopita.

Hata hivyo ,aliomba watu waweke vitambulisho vyao karibu ili wanapopita makarani waweze kujua idadi ya wenye vitambulisho huku mamlaka husika iweze Kuwa na takwimu halisi ya walivyo navyo na wasio navyo, vilevile ,alitoa Rai kwa jamiii kuacha kuwaficha walemavu na badala yake wahesabiwe ili kupata taarifa sahihi ya idadi na aina ya ulemavu walionao.

Kuhusu Wamachinga wameingizwa katika sensa, Ni kundi muhimu, ambapo Serikali inataka kujua idadi halisi,wenye vitambulisho kwani mpango wa Rais Samia Suluhu Hassan ni WAMACHINGA kupatiwa vitambulisho vya ujasiliamali.

"Tushiriki kikamilifu, na Baadhi ya maswali yatakayoulizwa na makarani wa Sensa ni elimu ya wanakaya, shughuli zao za kiuchumi, hali ya uzazi, taarifa za vifo na vifo vitokanavyo na uzazi,ajira, makundi maalum"alisema Anne.

Pamoja na hayo ,aliliasa kundi la vijana wakati wakitumia mitandao kuchat pia watumie wasaa huo kuhamasishana kuhusu suala la umuhimu wa Zoezi la sensa ili kutambua vijana waliopo na taarifa zao kuhusiana na suala la ajira.

Mkuu wa mkoa wa Pwani  Abubakari Kunenge alieleza, mkoa umejipanga Kuwa sehemu ya mafanikio Kwenye Zoezi la sensa .

Alielezea kwamba ,zaidi ya viongozi wa dini 1,500 kutoka madhehebu na nyumba za ibada mbalimbali wameshiriki kwenye kongamano hilo la viongozi wa dini.

Kunenge alisema, mkoa na wilaya umejiwekea mikakati kuanzia vitongoji ,kata,wilaya na mkoa kutoa elimu ya umuhimu wa sensa kupitia njia mbalimbali ikiwemo mikutano na wananchi,bodaboda,wakufunzi,makarani,matamasha ,kwenye michezo na makongamano .

"Watendaji 143 nao wameudhuria mafunzo ili kupata uelewa wa kusimamia Zoezi la sensa;"Pamoja na vikao viwili vya kamati ya sensa mkoa vimefanyika "alieleza Kunenge.

Kwa upande wake,Mwenyekiti mwenza wa kamati ya Usalama mkoa ambae pia ni Sheikh mkuu mkoa wa Pwani Hamis Mtupa sensa Ni takwa la kidini.

"Mafanikio pia ya kidunia Ni kwasababu ya kujisensa mwenyewe kwahiyo sensa Ni agizo na takwa la kidini ili kujua kesho yako.

Mtupa alieleza kuwa, viongozi wa dini wamelibeba Zoezi hili watahakikisha linafanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Nae Askofu Emmanuel Mhina alisema kuwa kamati hiyo ilianza kipindi kirefu kufanya maandalizi ya kongamano hilo na hadi sasa wanaona kuna mwelekeo mzuri.

"Tunaona kuna mafanikio makubwa hadi hapa tulipofikia mwitikio ni mkubwa hivyo tunaamini kuwa siku ya sensa wananchi watajitikeza kuhesabiwa"alisema Mhina.

Mchungaji wa Kanisa Anglikana Kibaha Mkoani Pwani Exavia Mpambichile aliwataka Waumini na wakazi wa Mkoa huo kuzingatia maagizo ya Serikali na kujitokeza wakati wa Sensa Ili kupatikana takwimu sahihi itakayofanikisha Serikali kupanga bajeti stahiki .

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.