• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Aanika Mikakati ya Kuongeza Mapato na Usimamizi wa Miradi Mafia.

Posted on: August 14th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Pili Mnyema, ameanza ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia leo, Agosti 14, 2025, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kutembelea Halmashauri zote za Mkoa wa Pwani.  Lengo la ziara hiyo ni kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kufanya vikao kazi na watumishi wa Halmashauri husika.

Akiwa katika ziara hiyo, Mnyema amewataka viongozi wa Halmashauri ya Mafia kujifunza kutoka maeneo mengine yenye mazingira yanayofanana kijografia lakini yamepiga hatua kubwa kiuchumi, ili kuboresha ubunifu wa miradi na kuongeza mapato ya Halmashauri.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kukamilisha miradi kwa wakati, kuepuka uzembe katika usimamizi na kuhakikisha utunzaji wa vifaa hususan vya afya, ili kuongeza tija kwa wananchi.

“Serikali inajitahidi sana katika kampeni ya kupunguza vifo vya mama na mtoto, hivyo ni wajibu wetu kuunga mkono juhudi hizo kwa kujituma, kutimiza majukumu yetu na kutunza vifaa tulivyonavyo,” alisema Mnyema.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Mhe. Petro Magoti, amewataka watendaji kufanya kazi kwa bidii na kujituma hususan katika usimamizi wa miradi ya maendeleo, ili iwanufaishe wananchi na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kukuza maendeleo ya Taifa.

Ameongeza kuwa kuanzia Jumamosi atarejea wilayani humo kufuatilia maendeleo ya miradi inayoendelea kukamilishwa pamoja na utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa na Katibu Tawala.

“Hatucheki na mtu kwenye miradi. Kuanzia Jumamosi nitakuwa hapa kuhakikisha mambo yote yaliyoanishwa yanatekelezwa,” alisema Mhe. Magoti.

Katika ziara hiyo, Katibu Tawala alikagua miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa soko la Kilindoni lenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 700, ujenzi wa jengo la wazazi katika Hospitali ya Wilaya lenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 500, pamoja na maboresho ya majengo ya Shule ya Msingi Utende yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 85.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Bagamoyo Yatangazwa Rasmi Kuwa Halmashauri ya Mji – Serikali Kupeleka Zaidi ya Milioni 1,000 kwa Miradi ya Maendeleo.

    August 22, 2025
  • Mchengerwa Atoa Wito kwa Watumishi wa Afya Kuhudumia Wananchi kwa Upendo,

    August 22, 2025
  • Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Aanza Ziara ya Kikazi Kisarawe, Akagua Miradi na Kusisitiza Uwajibikaji.

    August 18, 2025
  • Mradi wa Mifumo ya Umeme Jua na Usamabazaji wa Majiko Banifu kwa Bei ya Ruzuku waanza Mkoani Pwani.

    August 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.