• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Katibu Tawala Pwani Azitaka Halmashauri za Bagamoyo na Chalinze Kudhibiti Matumizi ya Fedha za Umma.

Posted on: June 18th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Rashid Mchatta, amezielekeza Halmashauri za Bagamoyo na Chalinze kusimamia kwa umakini matumizi ya fedha za umma ili kuepusha hoja zinazotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Mchatta alitoa maagizo hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, katika vikao vya Baraza la Madiwani vilivyofanyika kwenye halmashauri hizo, kwa ajili ya kupitia na kujadili hoja zilizotolewa kwenye ripoti ya CAG kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Katika hotuba yake, Mchatta alizipongeza Halmashauri hizo kwa kufanikisha ukusanyaji wa mapato na kuvuka malengo yaliyowekwa. Aidha, alizitaka kuhakikisha kuwa hoja zote zilizosalia zimefungwa ifikapo tarehe 30 Septemba 2025, sambamba na kuongeza wigo wa mapato kwa kubuni vyanzo vipya vya mapato.

“Imarisheni usimamizi wa mapato ya ndani kwa kudhibiti mianya ya upotevu, kwa mfano kwa kufunga kamera za CCTV katika maeneo kama stendi za mabasi na sehemu nyinginezo zinazohusisha mapato ya moja kwa moja,” alisisitiza Mchatta.

Katika vikao hivyo, Halmashauri ya Bagamoyo na ile ya Chalinze zilipongezwa kwa kupata hati safi kutoka kwa CAG, ikiwa ni ishara ya usimamizi mzuri wa fedha za umma na uwajibikaji wa viongozi wa halmashauri hizo.

Kwa upande wao, wakurugenzi wa Halmashauri hizo walieleza kuwa walifanikiwa kujibu hoja zote zilizotolewa katika ripoti ya CAG, hali iliyosaidia kuimarisha uwazi na nidhamu ya matumizi ya fedha za serikali.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze, Hassan Mwinyikondo, alisisitiza umuhimu wa kudhibiti mapato ya halmashauri na kuhakikisha matumizi yake yanaendana na bajeti iliyopitishwa, ili kuepusha hoja zisizo za lazima.

Naye Pastory Massawe, Mwakilishi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mkoa wa Pwani, aliwapongeza madiwani kwa kusimamia halmashauri hadi kupata hati safi. Hata hivyo, alisisitiza umuhimu wa kuzuia hoja mpya badala ya kuwa wazuri tu wa kujibu hoja.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Katibu Tawala Pwani Azitaka Halmashauri za Bagamoyo na Chalinze Kudhibiti Matumizi ya Fedha za Umma.

    June 18, 2025
  • Siamini katika kushindwa - RC Kunenge.

    June 17, 2025
  • Kunenge: Pangeni Vipaumbele vyenye tija kwa Jamii.

    June 16, 2025
  • Kaimu Katibu Tawala Msaidizi atoa wito kwa jamii Kuwalinda Watoto na Kuhakikisha malezi bora

    June 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.