• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kinondoni, FARMBASE na TARI Waibuka Kidedea Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki 2025

Posted on: August 8th, 2025

Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, kampuni ya FARMBASE Ltd, na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) wameibuka vinara katika Maonesho ya Kilimo ya Nane Nane Kanda ya Mashariki 2025 yaliyofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere, Morogoro.

Kinondoni iliongoza kwa kishindo katika kundi la Halmashauri, FARMBASE Ltd ikang’ara kama mshindi bora upande wa kampuni za zana za kilimo, huku TARI ikionesha umahiri mkubwa katika kundi la taasisi za utafiti wa kilimo. Ushindi wa taasisi hizo umetokana na ubunifu wa hali ya juu, matumizi ya teknolojia rahisi na rafiki kwa wakulima, pamoja na uwezo wao wa kufikisha elimu ya kilimo kwa ufanisi kwa wakulima na wananchi waliotembelea mabanda yao.

Maonesho haya yaliyojumuisha jumla ya washiriki 138 kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Tanga, yalilenga kuhamasisha matumizi ya teknolojia za kisasa katika kilimo na kutoa jukwaa la mafunzo kwa wakulima wadogo, vijana, wanawake na wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo.

Washiriki waligawanywa katika makundi 15 kulingana na asili ya taasisi zao, yakiwemo mashirika ya serikali, sekta binafsi, mashirika ya kimataifa, taasisi za fedha, na vyama vya wakulima. Kila kundi lilipimwa kwa kutumia vigezo mbalimbali vya kitaalamu ikiwemo ubora wa banda, ujumbe wa maudhui, na namna walivyoshirikisha makundi maalum kama vijana na wanawake.

Akikabidhi vikombe vya ushindi kwa taasisi zilizofanya vizuri, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Batilda Burian, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kilele cha maonesho hayo, aliwapongeza washiriki wote kwa kushiriki kikamilifu na kuonesha ubunifu mkubwa.

“Nimevutiwa sana na teknolojia zilizobuniwa na vijana, wanawake, na vikundi vya uzalishaji. Mbinu walizoonesha zimejikita katika kuongeza thamani ya mazao, kupunguza hasara baada ya kuvuna, na kuchochea kilimo biashara,” alisema Mhe. Burian.

Alitoa wito kwa washiriki wengine kuendelea kuboresha huduma na mawasilisho yao ili waweze kujipatia ushindi katika maonesho yajayo.

Maonesho ya mwaka huu yaliendeshwa chini ya kaulimbiu isemayo: “Chagua kiongozi boro kwa Maendeleo Endelevu ya kilimo, mifugo na Uvuvu"

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Bagamoyo Yatangazwa Rasmi Kuwa Halmashauri ya Mji – Serikali Kupeleka Zaidi ya Milioni 1,000 kwa Miradi ya Maendeleo.

    August 22, 2025
  • Mchengerwa Atoa Wito kwa Watumishi wa Afya Kuhudumia Wananchi kwa Upendo,

    August 22, 2025
  • Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Aanza Ziara ya Kikazi Kisarawe, Akagua Miradi na Kusisitiza Uwajibikaji.

    August 18, 2025
  • Mradi wa Mifumo ya Umeme Jua na Usamabazaji wa Majiko Banifu kwa Bei ya Ruzuku waanza Mkoani Pwani.

    August 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.