• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Mapato ya Korosho , Ufuta yaboreshe maisha ya Wananchi-RC Kunenge

Posted on: February 7th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakar Kunenge amewaasa wakazi wa mkoa huo kuhakikisha kuwa tija ya uzalishaji Korosho na ufuta iakisi maisha ya wananchi mkoani humo yanabadilika na kuwa bora.

Akifungua mkutano wa wadau wa Korosho na ufuta kupitia tathmini ya maendeleo ya uzalishaji mazao hayo leo Februari 7, 2023 kwenye ukumbi wa "Flexi Garden Hotel" Wilayani Mkuranga, Kunenge aliwaasa wakazi wa mkoa huo kujipanga kutumia fursa ya ardhi yenye zaidi ya ekari laki 4.5 zilizopo wilayani Rufiji zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za kilimo.

Katika kuendelea kuongeza uzalisha wa Korosho, Mkuu huyo wa mkoa aliwataka wakurugenzi wa halmashauri mkoani humo kutenga na kutoa pesa za ununuzi wa vitalu huku akiwaelekeza wakuu wa wilaya kuorodhesha na kumpatia taarifa ya idadi ya ekari za ardhi na mahala zilipo zilizotengwa kwa ajili ya kwa ajili ya kuanzisha mashamba mapya ya Korosho akitolea mfano wa Halmashauri ya wilaya ya Rufiji ambayo tayari imetenga zaidi ya ekari 500.

Awali, mkuu wa wilaya ya Mkuranga Khadija Nassir mbali na kueleza kuwa hakuna mkulima wa korosho wala ufuta anaedai malipo ya mazao waliyouza, pia alitaja baadhi ya changamoto kuwa ni mbadiliko ya tabia nchi ambayo alisema tafiti zinahitajika kukabiliana nayo ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha wakulima huku akishauri mashirika ya Bima kuwa na uhakika wa kufidia wateja wao iwapo mazao yao yatakumbwa na changamoto.

Akizungumzia wakulima wa mazao ya korosho na ufuta, Nassir aliomba wasafirishaji wa vifungashio wawe wanashusha vya wilaya yake Mkuranga mjini badala ya kuvipeleka Rufiji.

Kwa upande wake Afisa Kilimo mkoa huo Jerry Mgonja akitoa taarifa alisema uzalishaji wa zao la ufuta mwaka 2021/2022 aliongezeka kufikia tani 11,629 na mauzo yalifanyika kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.

Kuhusu uzalishaji wa zao la korosho Mgonja alieleza kuwa umeimarika kutoka tani 70,733 kwa mwaka 2020/2021 hadi tani 15,862 mwaka 2021/2022 huku ubora wa daraja la kwanza ukipanda kutoka asilimia 12 hadi 72.

Naye Meneja Mkuu wa chama kikuu cha ushirika cha mkoa wa Pwani (CORECU) Hamisi Mantawela alisema wameendesha minada tisa ya korosho yenye tani 10,759,499 zilizouzwa kwa stakabadhi ghalani na tani 1,391,840 ziliuzwa kwa wabanguaji wa ndani.

Akitoa salaam za Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) Francis Alfred aliwahimiza wakulima kusafisha mashamba yao wakati bodi hiyo ikiendelea na kujipanga tayari kwa ugawaji wa pembejeo.




Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.