• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Pwani yajipanga kumaliza Chanjo na Utambuzi wa Mifugo ndani ya siku 30

Posted on: July 9th, 2025

Mkoa wa Pwani umeweka rekodi ya kipekee kwa kujipanga kutekeleza zoezi la chanjo na utambuzi wa mifugo ndani ya kipindi kifupi cha siku 30 pekee, tofauti na muda wa miezi miwili uliopangwa kitaifa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Ahadi hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mhe. Shaib Ndemanga, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Pwani katika ziara ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, katika kijiji cha Miono, Wilaya ya Chalinze. Ziara hiyo ililenga kukagua utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo.

“Tunajua nyie kama Wizara mmepanga kutekeleza awamu ya kwanza ya zoezi hili kwa miezi miwili, lakini nikuhakikishie Mhe. Waziri, Mkoa wa Pwani kwa furaha tuliyonayo na namna tulivyopokea zoezi hili, tutahakikisha tunamaliza ndani ya siku 30,” alisema Mhe. Ndemanga kwa msisitizo.

Kwa upande wake, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, amepongeza uongozi na wananchi wa mkoa wa Pwani kwa kujitokeza kwa wingi na kupokea kampeni hiyo kwa uzito unaostahili, akisema ni sehemu ya kutekeleza maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuimarisha sekta ya mifugo.

“Tunaendelea na majadiliano na nchi tano ambazo zinaonesha nia ya kuchukua mifugo yetu ikiwa hai. Hii inadhihirisha kuwa soko la mifugo lipo, na hapa Pwani tuna kiwanda kikubwa cha kuchakata nyama ambacho sasa kinaweza kufikia uwezo wake wa asilimia 100, tofauti na sasa ambapo kinafanya kazi kwa asilimia 50,” alifafanua Mhe. Dkt. Kijaji.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Mkoa wa Pwani, Bw. Ngobere Msamau, ameishukuru serikali kwa kuwaletea chanjo hizo, huku akiahidi kuwa wafugaji wataendelea kufuata maelekezo na ushauri wa serikali kutokana na manufaa wanayoanza kuyaona.

Ziara ya Mhe. Dkt. Kijaji ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo, iliyoanzishwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 16 Juni 2025 katika Wilaya ya Bariadi, mkoa wa Simiyu. Kampeni hiyo inaendelea katika mikoa mingine, ikiwemo Morogoro ambapo Waziri atazuru tarehe 10 Julai 2025.



Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Waziri Mchengerwa aipongeza Shule ya Sekondari ya wavulana Kibaha kwa Ufaulu wa Kiwango cha Juu

    July 10, 2025
  • Mkoa wa Pwani na Program ya Shule Bora waimarisha uelewa wa mabadiliko ya Tabianchi kwa Wataalam wa Halmashauri

    July 09, 2025
  • Pwani yajipanga kumaliza Chanjo na Utambuzi wa Mifugo ndani ya siku 30

    July 09, 2025
  • Maafisa Habari Pwani Wqashiriki Warsha ya Mawasiliano ya Kimkakati kupitia Program ya Shule Bora.

    July 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.