• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

Posted on: May 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mheshimiwa Abubakar Kunenge, amesema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ameendelea kuwa mfano bora wa kuigwa katika utendaji kazi, na hivyo kuwataka wafanyakazi wote nchini kuiga mfano huo.

Kunenge aliyasema hayo leo katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika katika uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha, mkoani Pwani.

Alisema kuwa Rais Samia amekuwa mstari wa mbele katika kutatua changamoto za wananchi, jambo linalopaswa kuwa dira kwa wafanyakazi wote.

“Niwaambie, Mheshimiwa Rais ni mfanyakazi namba moja. Tunamwona anafanya kazi bila kupumzika, ametuwekea sera nzuri ambazo tunaona matokeo yake katika huduma bora za afya, elimu, uwekezaji, kilimo, mifugo, maji na miundombinu mingine. Hivyo basi, tusimuangushe,” alisema Kunenge.

Aidha, aliwataka watumishi wa sekta ya umma na binafsi kutokuwa na moyo wa kushindwa, akisisitiza kuwa hata Rais haamini katika kushindwa.

“Mhe. Rais haamini katika kushindwa, mimi pia siamini katika kushindwa, na Mkoa wangu hauamini katika kushindwa,” aliongeza.

Kuhusu maendeleo ya Mkoa, Kunenge alisema kuwa katika kipindi cha miaka mitano, mkoa wa Pwani umepokea shilingi trilioni 1.53 kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Alisema fedha hizo zimetumika kuboresha sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu na miundombinu.

Akizungumzia sekta ya viwanda, Kunenge alieleza kuwa mkoa huo una zaidi ya viwanda 1,500, ikiwa ni pamoja na viwanda vikubwa 78 ambavyo vimechangia kuongeza ajira kwa wananchi.

Aidha, alieleza kuwa mkoa umeanza mazungumzo na wawekezaji kuhusu utoaji wa mikataba ya ajira kwa wafanyakazi pamoja na kuwahimiza wachangie kwenye mifuko ya jamii.

Akijibu risala ya wafanyakazi, Kunenge alitoa wiki moja kwa kila taasisi iliyotajwa kwenye risala hiyo kuwasilisha majibu ya changamoto zilizowasilishwa, hasa kuhusu mikataba ya ajira.

“Kama mikataba haipo, tujue ni nani anayesimamia. Ninachotaka kuona ni mikataba kuwepo na kila kero iliyotajwa hapa kuwa na majibu,” alisema Kunenge.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TUCTA Mkoa wa Pwani, Ramadhani Kinyogori, alishukuru Rais kwa kuendelea kutatua changamoto za wafanyakazi nchini.

Awali, akisoma risala ya wafanyakazi, Mratibu wa TUCTA Mkoa wa Pwani, Bi. Susan Shesha, aliipongeza Serikali kwa kusikiliza na kutekeleza uanzishaji wa mabaraza ya wafanyakazi katika wilaya zote za mkoa huo, na pia kutoa huduma bora kwa watumishi mahala pa kazi.

Hata hivyo, Shesha alitaja changamoto zinazowakabili wafanyakazi kuwa ni pamoja na mishahara isiyoendana na hali halisi ya maisha, baadhi ya waajiri kukiuka mikataba ya ajira, kuwazuia wafanyakazi kushiriki sherehe za Mei Mosi, na kutotoa michango katika mifuko ya jamii.

Alisisitiza kuwa vyama vya wafanyakazi vinawaomba waajiri kutimiza wajibu wao na kuongeza kasi ya kulipa madeni ili kuepusha migogoro kazini.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.