• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

Posted on: April 30th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, leo ameuagiza uongozi wa Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) kutafuta na kufanyia kazi hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyoitoa Aprili 28, 2025 jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa Benki ya Ushirika.

Mhe. Kunenge alitoa agizo hilo wakati akifungua Mkutano wa 31 wa Mwaka 2024/25 wa CORECU uliofanyika katika Ukumbi wa Destiny, Kibaha kwa Mathias, Mkoa wa Pwani.

“Agizo langu kwenu, uongozi wa CORECU, ni kutafuta hotuba ya Mhe. Rais aliyoitoa Dodoma kwenye uzinduzi wa Benki ya Ushirika na kufanyia kazi maono yake ili kuendeleza Ushirika,” alisema Mhe. Kunenge.

Akiendelea, alisisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa bidii na kwa matokeo ili kumuenzi Rais Samia, akibainisha kuwa mkoa wa Pwani hauamini katika kushindwa.

“Mhe. Rais haamini katika kushindwa. Mimi, mlezi wenu, siamini katika kushindwa, na Mkoa wa Pwani pia hauamini katika kushindwa. Tumpe heshima Rais kwa kufanya kazi zitakazowasaidia wananchi,” aliongeza Mhe. Kunenge.

Vilevile, Mkuu huyo wa Mkoa aliwapongeza viongozi wa CORECU kwa kufanya kazi kwa uadilifu na kuwataka wasisite kuwachukulia hatua watu wanaokiuka sheria kwa kutorosha mazao kama korosho na ufuta.

“Korosho na Ufuta ni uti wa mgongo wa uchumi wa mkoa huu. Tusiwavumilie watu wanaotorosha mazao. Nimetoa maagizo kwa Wakuu wa Wilaya kuchukua hatua kali kwa watakaobainika,” alisisitiza.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Kanali Joseph Kolombo, alisema wilaya yake ipo katika hatua ya palizi za mikorosho na kuagiza maafisa ugani kufuatilia kwa ukaribu idadi ya mikorosho kwa kila kata, hatua inayosaidia kuifanya Kibiti kuongoza kwa uzalishaji wa zao hilo.

Akitoa taarifa ya utekelezaji, Mwenyekiti wa Bodi ya CORECU, Musa Hemed Mng’eresa, alisema kwa mwaka 2024/2025, chama hicho kimefanikiwa kuuza ufuta tani zaidi ya 13,000, mbaazi tani 295.7 na korosho kilo 19,989,228, na hivyo kufanikisha mauzo yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 67.

Aidha, alimpongeza Rais Samia kwa kuwezesha upatikanaji wa pembejeo, hali iliyochangia ongezeko kubwa la uzalishaji kwa wakulima.

Naye, Mrajisi Msaidizi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Bw. Mutaabazi, alisema mkoa huo una jumla ya vyama vya ushirika 202, ambapo 162 kati yake ni hai. Aliongeza kuwa wakulima 137,000 tayari wamesajiliwa kupitia mfumo wa MUVU.

Akizungumzia mafanikio, alisema vyama hivyo sasa vimeanza kutumia mifumo ya TEHAMA katika usajili na pia kujenga maghala ya kuhifadhi mazao yao.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.