• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge ahimiza Ushirikiano Kati ya Serikali na Sekta Binasfi kukuza Biashara na Uwekazaji

Posted on: October 2nd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi ili kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji.

Kunenge alitoa wito huo Oktoba 2, 2024 wakati wa kikao cha majadiliano kati ya sekta binafsi (PPD) na serikali kilichofanyika leo katika Ofisi za Mkoa wa Pwani.

Akizungumza katika kikao hicho, Kunenge alisema ushirikiano huo utawezesha kutambua changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara, na hivyo serikali kuweza kuweka mazingira rafiki ya kukuza biashara na kuongeza uwekezaji.

"Lazima tushikamane kati ya sekta binafsi na serikali ili kuweza kujua wapi tunafanya vizuri na changamoto zilizopo ili kuhakikisha tunaboresha mazingira ya biashara na uwekezaji," alisema Kunenge.

Pia aliwataka wafanyabiashara kuhakikisha wanachangia kuongeza mapato ya serikali na kuboresha biashara zao kwa kutumia fursa mbalimbali zinazowezesha ukuaji wa biashara na uwekezaji kwa kufanya mambo tofauti na waliyozoea.

Aidha, Kunenge aliwaasa wafanyabiashara na wawekezaji kufuata matakwa ya kisheria ili kuweka mazingira bora yanayowezesha serikali kutoa msaada stahiki.

Alisisitiza maafisa biashara kufanya kazi kwa weledi ili kuleta matokeo chanya, akiongeza kuwa, "Tumia fursa unapopewa nafasi, na uhakikishe unachokifanya kinaonekana."

Kwa upande wake, Mwenyekiti (ni nani)wa Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani alishauri serikali kutoa elimu kwa walipa kodi kabla ya kuwakamata na kuwatoza faini, akisema kuwa hatua hiyo inachangia wafanyabiashara wengi kupoteza mitaji yao na kusababisha biashara zao kufa.

Alipendekeza pia serikali kutengeneza huduma wezeshi mkoani, kama vile masoko, ili kuvutia wafanyabiashara wengi zaidi.

Naye Mwenyekiti wa Jumuia ya Wafanyabiashara (JWT) Mkoa wa Pwani, Abdallah Ndauka, alitoa wito kwa maafisa biashara wa mkoa na halmashauri kuwasaidia wakurugenzi kutambua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara na kuziwasilisha kwa viongozi ili kuweka mazingira rafiki ya kutatua changamoto hizo na kuepusha migogoro isiyo ya lazima.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.