• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge aishauri TENMESA Kushugulikia maoni ya Wadau kwa Wakati

Posted on: September 24th, 2023

Mkuu wa mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, amewataka TEMESA kushughulikia kwa wakati maoni ya wadau zikiwemo taasisi za watu binafsi ambazo hufika ofisini kwao kwa ajili ya kupata huduma.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Mhe. Meja Edward Gowelo alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakari Kunenge kwenye kikao kilichowahusisha TEMESA na wadau wake zikiwemo Taasisi za serikali na za watu binafsi kilichofanyika Halmashauri ya Mji Kibaha mkoani Pwani.

Kwenye kikao hicho, Mkurugenzi wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania TEMESA, Lazaro Kilahala amesema katika kuhakikisha wanaboresha huduma zao tayari wanazo karakana 21 nchini ambazo zinatoa huduma kwa ubora unaotakiwa huku 13 zikifanyiwa marekebisho.

Amesema majukumu ya TEMESA ni kufanya matengenezo ya magari, pikipiki, usimikaji wa mitambo ya umeme, kusimamia na uendeshaji wa vivuko na kukodisha mitambo ya ujenzi.

Ameongeza kuwa tayari wamekamilisha vivuko 32 nchini ambavyo vinafanya kazi na wananchi wanapata huduma muda wote lakini pia wanaendelea na maboresho ya upatikanaji wa huduma.

Amesema serikali imetoa fedha nyingi kwa ajili ya kusaidia wakala huyo kutoa huduma nzuri kwa wananchi hivyo anategemea wataendelea kuboresha kulingana na mahitaji wa watu.

Akibainisha maboresho yanayofanyika kwenye taasisi hiyo, Mkurugenzi wa Matengenezo wa TEMESA Hussein Hassan amesema kuwa wamechukua uamuzi wa kuwapeleka mafundi wake 50 kwenye vyuo mbalimbali kujifunza mbinu za kisasa za utengenezaji wa vyombo vya moto ili kuepusha malalamiko kwa wateja wao.

Hassan amesema wameamua kuwapeleka vyuoni mafundi hao baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa wateja wakidai baadhi ya magari yanashindwa kutengenezwa ipasavyo au kuchelewa kutokana na matoleo mbalimbali ambayo upatikanaji wa vifaa vyake ni changamoto na utengenezaji wake unahitaji ujuzi zaidi.

Kutokana na hali hiyo, amesema wamepeleka vyuoni kujifunza na baada ya kuhitimu watakuwa mafundi wazuri ambao wataweza kutengeneza magari kwa ubora unaotakiwa na kwa muda mfupi ukilinganisha na ilivyokuwa awali.

“Hatua hii ni sehemu ya maboresho yetu, sisi TEMESA kupitia kitengo chetu cha huduma kwa wateja tulipokea maoni mengi likiwemo suala la uchelewaji wa ukarabati na utengenezaji wa magari, ifahamike kuwa kila mara kunakuwa na matoleo mapya ya magari, sasa ili tukidhi mahitaji ya wateja wetu ni vyema tukawa na ujuzi na teknolojia ya kutosha ili kila gari tuweze kulihudumia,” amesema Hassan.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.