• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge awataka Viongozi Mkoa Pwani Kusimamia utunzaji Misitu

Posted on: April 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amewaelekeza Viongozi wa Wilaya, Halmashauri na Wakala wa Huduma za Misitu mkoani humo kuzingatia utunzaji wa misitu iliyohifadhiwa kwa kuzuia uharibifu wa misitu ili kuhifadhi mazingira.

Maelekezo hayo ya Mkuu wa Mkoa yametolewa kwa niaba yake Mjini Kibiti April 9, 2024 katika siku ya upandaji miti kimkoa na Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo.

Amesema kuwa viongozi wa Vijiji wanapogawa au kuuza maeneo wahakikishe hawaingilii yale yenye misitu hata kama hayajahifadhiwa kisheria.

"Zuieni uchomaji mkaa, uvamizi wa Mifugo, uchimbaji wa michanga, kokoto kilimo na kuweka makazi katika maeneo hayo kwani ongezeko la watu na ukosefu wa nishati ni moja ya mambo yanayotoa msukumo wa mahitaji ya mazao ya misitu ikiwemo kuni, mkaa na maeneo ya makazi hivyo kusababisha kuongezeka kwa ukataji na ufyekaji wa misitu," amesema.

Katika maelekezo hayo amesema kuwa endapo Serikali za Vijiji, Wilaya, Halmashauri na Taasisi nyingine zitasimamia maelekezo hayo itaimarisha ulinzi na usimamizi wa misitu kwenye maeneo yao.

Pia amesisitiza kuwa kila Halmashauri za mkoa huo ziwe zinapeleka taarifa ya maendeleo ya miti iliyopandwa mwaka kila mwaka na kueleza idadi ya miti ikiwa ni pamoja na mingine iliyokufa.

Kanal Kolombo amesema katika kipindi cha mwaka 2022/2023, mkoa wa Pwani ulipanda miti 8,876,640 na katika msimu huu wa 2023/2024 miche 10,436,494 imezalishwa na inaendelea kupandwa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo.

"Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani nawasilisha maelekezo haya ya kila Halmashauri kuhakikisha wanafikia malengo ya Serikali kupanda miti Milion 1.5," amesema Kanali Kolombo.

Akizungumza kwa niaba ya Kamanda wa Kanda ya Mashariki, Mhifadhi Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) Shabani Kiula amesema majukumu waliyonayo ni kuhakikisha misitu inaendelea kuhifadhiwa na wanaendelea kutoa miche aina mbalimbali bure ili watanzania wapate na kupanda kwenye maeneo yao.

Naye Afisa misitu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Pierre Ntiyamagwa amesema pamoja na upandaji miti pia wanakabiliana na uharibifu wa rasilimali misitu na uhifadhi wa mazingira.

"Hatua zulizochukuliwa ni pamoja na kufanya doria zinazoendesha na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) Kanda ya Mashariki kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya, kuongeza mwamko wa uanzishwaji wa vitalu vya niche na upandaji miti kwenye Asasi za kiserikali na zisizo za kiserikali," amesema.

Ameongeza kuwa vipo vikwazo vinavyoikabili rasilimali ya misitu akivitaja kuwa ni pamoja na ongezeko la idadi ya wakazi wa Mkoa wa Dar es Salam ambalo husababisha mahitaji makubwa ya kuni na mkaa na hivyo kuongezeka kwa ukataji na ufyekaji misitu na mapori mkoani humo.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.