• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

Posted on: April 25th, 2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amesisitiza umuhimu wa kuuenzi na kuulinda Muungano wa Tanzania, akisema kuwa Muungano huo ni kichocheo kikubwa cha maendeleo ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na kitamaduni kwa Taifa.

Akizungumza leo na wananchi wa Mkoa wa Pwani katika ziara yake ya siku moja, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Miaka 61 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika Kibaha Shopping Mall, Dkt. Tulia alisema Muungano umejenga msingi wa mshikamano na umoja miongoni mwa Watanzania.

“Tanzania inaendelea kuwa kisima cha amani na inatambulika dunia nzima. Muungano huu umechangia kwa kiasi kikubwa kutufanya tuwe na sauti moja na kutambulika kimataifa. Umenisaidia hata mimi kuweza kushika nafasi ya Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani,” alieleza Mhe. Dkt. Tulia.

Alisisitiza kuwa ingawa vijana wengi hawakushuhudia kuasisiwa kwa Muungano huo, ni wajibu wao kuuenzi na kuudumisha kwa kuzingatia matendo na maneno yanayoujenga na kuulinda.

“Watanzania tuulinde Muungano kama vile waasisi wetu walivyofanya. Vijana kama sisi hatukuwepo enzi hizo, lakini Muungano tumeukuta na tunaendelea kuudumisha. Niwasihi tufakari matendo na maneno yetu ili yawe na mchango chanya kwa Muungano wetu,” alisisitiza.

Katika hotuba yake, Dkt. Tulia pia alizungumzia maboresho ya sheria ya ukaguzi yaliyofanywa kwa kuzingatia maoni ya wananchi na wadau, akieleza kuwa mabadiliko hayo yamechochewa na falsafa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia dhana ya “4R” (Reconciliation, Resilience, Reforms, Rebuilding).

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete, alieleza kuwa Muungano umekuwa chachu ya maendeleo, hasa katika kudumisha mahusiano mazuri baina ya Tanganyika na Zanzibar ambayo yamechangia kwa kiasi kikubwa ustawi wa Mkoa wa Pwani.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia imewekeza zaidi ya shilingi trilioni moja kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika mkoa huo. Alisema mkoa huo umekamilisha jumla ya viwanda vikubwa 78, na kufikisha idadi ya viwanda 1,553, vikiwemo 128 vikubwa.

“Yeyote anayetaka kuthibitisha utumishi uliotukuka wa Mhe. Rais aje Mkoa wa Pwani. Pwani imefunguka kwa juhudi za Mhe. Rais, na pia amekuwa mfano bora kwa watoto wa kike katika kufanya vizuri mashuleni,” alisema Mhe. Kunenge.

Kaulimbiu ya maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano mwaka huu ni: “Muungano Wetu ni Dhamana, Heshima na Tunu ya Taifa – Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.”

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.