• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

TFS yakabidhi mil.20 kusaidia changamoto mafuriko Rufiji

Posted on: April 25th, 2024

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imetoa kiasi cha Sh. milioni 20 kwa ajili ya kusaidia kutatua Changamoto za wahanga wa mafuriko yaliyotokea katika Wilaya ya Kibiti na Rufiji Mkoani Pwani.

Mfano wa hundi ya fedha hizo imekabidhiwa leo na meneja mahusiano wa TFS nchini Johary Kachwamba kwa mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge katika hafla iliyofanyika ofisi za Mkuu huyo zilizopo Mjini Kibaha.

Kachwamba, amesema kuwa TFS kupitia Kamishna wake Silayo Dos Santos imeguswa na janga hilo la mafuriko ndio maana imeona kuna kila sababu ya kuunga mkono Serikali kwa kusaidia wahanga wa Wilaya hizo.

Amesema kuwa TFS kwa eneo la Rufiji wanamisitu na kwamba wana - Rufiji ni wahifadhi wenzao kwa kuwa TFS ina misitu zaidi ya 10 ikiwa na zaidi ya hekta 32,000 ndio maana Kamishna wa Uhifadhi ameridhia kutoa kiasi hicho ili kusaidia wahanga hao.

Amesema kuwa pamoja na kutoa mchango huo, bado TFS itaendelea kuwashika mkono katika kutatua changamoto mbalimbali pale ambapo itahitajika kwa kuwa jambo hilo linahitaji ushirikiano wa pamoja.

"TFS kupitia Kamishna wa Uhifadhi Silayo Dos Santos imetoa kiasi cha Sh. milioni 20 kusaidia changamoto za wahanga wa mafuriko Rufiji na Kibiti lakini tutaendelea kushika mkono kulingana na mahitaji ," amesema Kachwamba.

Akizungumza mara baada ya kupokea hundi hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ameishukuru TFS kwa mchango huo kwani wameonyesha namna ambavyo wameguswa na janga la mafuriko hayo.

Kunenge, amesema kuwa TFS wamefanya jambo hilo kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kwamba kitendo hicho kinampa faraja Rais katika kuwatumikia Wananchi.

"Nawashukuru sana wenzetu wa TFS kwa kutoa mchango huu mkubwa kwa ajili ya kusaidia wahanga wa mafuriko Wilayani Kibiti na Rufiji, ni mfano wa kuigwa kwao kwakuwa wanaunga mkono Rais Samia," amesema Kunenge.

Mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa pamoja na kutoa mchango wa fedha hizo, TFS wameonesha moyo wa pekee kwani kabla ya kutoa fedha hizo tayari wametoa eneo na viwanja kwa ajili ya kufanyia shughuli za mafuriko.

Pia ameahidi kuzitumia fedha hizo katika kutoa huduma kwa wahanga wa mafuriko hayo huku akiwaomba TFS kuendelea kumuunga mkono Rais Samia na kuhakikisha wanatoka katika kutumia nishati ya mkaa na kwenda katika nishati mbadala.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.