• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Ujenzi Mradi wa maji Rufiji, Dar wapata Mkandarasi Mshauri

Posted on: February 13th, 2023

Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imepata mshauri mwelekezi kujenga bwawa kubwa kwenye Mto Rufiji eneo la Mloka ambalo litazalisha lita milioni 750 za maji kwa siku.

Hayo yalibainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakar Kunenge alipokuwa akizungumza na wakazi wa Fukayosi mara baada ya kuzindua upanuzi wa mradi wa maji kwenye kata ya Fukayosi Wilayani Bagamoyo ambao kwa mujibu wa Meneja wa RUWASA Wilaya ya Bagamoyo Mhandisi James Kionaumela umegharimu sh. milioni 350.3 mkandarasi akiwa ni Ms Shamoka Building and Civil Contructors Ltd. na utahudumia kaya 374 zenye watu 2,242 watakaopata huduma ya maji safi na Salama.

Alhaji Kunenge Alisema kuwa mradi huo wa Mloka Rufiji utasaidia kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji kwa mkoa wa Pwani na Dar es Salaam pia kwa ajili ya wawekezaji, kilimo cha umwagiliaji na kwa wafugaji.

Katika hatua nyingine, Alhaji Kunenge ameagiza mkandarasi Civil Loth anayetekeleza mradi wa bwawa la maji katika Kitongoji cha Mjembe Kijiji cha Kwa Mduma Kata ya Kibindu Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo kuripoti ofisini kwake kwa kushindwa kukamilisha mradi huo wenye thamani ya shilingi milioni 966 pamoja na kuwa aliomba na kuongezewa muda wa ziada wa miezi tisa.

Kunenge alisema mkandarasi huyo tayari alishalipwa kiasi cha shilingi milioni 483 sawa na asilimia 51.1 ya gharama za mradi lakini hajakamilisha kazi hiyo ambayo imefikia asilimia 73.

"Nilimpigia simu ili tukutane naye eneo la mradi lakini hajafika akidai yuko Mtwara namtaka aje ofisini Februari 16 ili atueleze changamoto yake ni nini inayomfanya ashindwe kukamilisha mradi kwa wakati licha ya kuongezewa muda," alisema Kunenge.

Akizungumzia mradi huo Meneja wa RUWASA Mkoa wa Pwani Mhandisi Beatrice Kasimbazi alisema kuwa changamoto kubwa ni mkandarasi huyo kutokuwa kwenye eneo la mradi huo wa Mjembe na Goe kwa muda mrefu na hata akiitwa kwenye vikao hafiki.

Kasimbazi aliongeza kuwa wanashindwa kuelewa mkandarasi huyo anakabiliwa na shida gani kwani wanapomwita kutaka kujua nini kinamkwamisha ili wamsaidie aweze kukamilisha mradi kwa muda aliopewa hatokei.

Diwani wa Kata ya Kibindu Ramadhan Mkufya alisema kuwa wananchi wa Kata hiyo kwenye Vijiji vyote wana shida kubwa ya maji hivyo mradi huo ungekuwa na manufaa makubwa kwao endapo ungekamilika.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.