• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Wananchi Kibaha watapeliwa zaid ta Sh Milioni 900 ununuzi wa Viwanja" feki".

Posted on: November 4th, 2023

Zaidi ya sh milioni 900, zimetafunwa na watu wanaodaiwa kuwa ni madalali na baadhi ya viongozi wa vitongoji wakati wa mauziano ya viwanja vya eneo la serikali la Mitamba shamba namba 34 lililopo Kata ya Pangani, Halmashauri ya Mji Kibaha mkoani Pwani.

Mkuu wa mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa kauli hiyo Novemba 3, 2023 kwenye kikao kilichowahusisha waandishi wa habari wa mkoa huo, wakuu wa wilaya, watalaam na wakurugenzi kutoka Halmashauri mbalimbali, kilichokuwa na lengo la kuwasilisha taarifa za utatuzi wa migogoro hasa ya ardhi.

Amesema eneo la Mitamba likiwa na shamba namba 34, lenye ukubwa wa hekta 4000 lilivamiwa na wananchi na kuendeleza shughuli zao.

Amesema maamuzi ya baraza la mawaziri lililokuwa na kazi maalumu ya kushughulikia migogoro ya ardhi nchini liliagiza waliovamia eneo hilo kuondoka mara moja.

Amesema licha ya kuwepo kwa uhalali wa serikali kupitia Wizara ya mifugo kumiliki eneo hilo lakini madalali waliendelea kuwauzia viwanja wananchi.

Hata hivyo, hivi karibuni katika mkutano wake na wananchi wa Kata ya Pangani, Kunenge alitoa muda wa siku 14 kukamatwa viongozi 24 wakiwemo mabalozi, wenyeviti wa mitaa, watendaji walioshirikiana na madalali waliohusika kuwauzia wananchi viwanja katika eneo la shamba namba 34 la Mitamba mali ya Wizara ya mifugo na uvuvi.

Kunenge alisema, anayo orodha ya majina ya viongozi na madalali waliohusika kuwauzia kinyemela wananchi viwanja katika eneo hilo ambalo linamilikiwa na serikali na kwamba anayakabidhi kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU pamoja na Jeshi la Polisi kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.

Aidha Kunenge alitoa agizo kwa Halmashauri ya Mji Kibaha, kupima eneo la shamba Namba 34 la Mitamba lenye ukubwa wa hekta 4000 na kubainisha mipaka yote na matumizi yake ili ijulikane kama vile eneo la ujenzi wa ofisi za umma na huduma za kijamii, makazi kabla ya kuanza oparesheni ya kuwaondoa wananchi walio ndani ya shamba hilo.

“Hekta 2963 kati ya 4000 zimerejeshwa kwa Halmashauri ya Mji Kibaha kwa ajili ya kutumika kwenye shughuli za maendeleo na kubakiwa na eneo la hekta 1037 ambazo hadi sasa zimebaki kwa Wizara ya Mifugo kwa ajili ya kufanya shughuli zake,” amesema Kunenge.

Siku chache zilizopita, alipozungumzia historia ya eneo hilo, Mpimaji Ardhi Halmashauri ya Mji Kibaha, Aron Shushu, alisema kiwanja hicho kilipimwa upya kwa kuzingatia sheria namba 8 ya mipango miji na kwamba mwaka 2021 kilifanyika kikao na wananchi hao kwa ajili ya kutoa katazo la kutovamia shamba hilo.

Katika taarifa yake Kunenge, amesema tayari waliohusika na utapeli wa kuuza shamba namba 34 wameanza kuripoti kwenye vyombo vya ulinzi na usalama kwa ajili ya hatua za kisheria.

Aidha amesema baadhi ya wananchi ni waoga kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili kuwashughulikia wale wote madalali waliouza kinyemele ardhi inayomilikiwa na serikali.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.