• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Mangula akitaka Kiwanda cha Biotech Productio Ltd kujitangaza

Posted on: June 18th, 2018

MAKAMU mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara ,Philip Mangula ameitaka bohari ya madawa (MSD) ,kuangalia namna ya kununua dawa ya viuadudu vya mazalia ya mbu,inayotengenezwa na   kiwanda cha Biotech kilichopo  Kibaha mkoani Pwani ili kuzuia malaria badala ya kupoteza mamilioni ya fedha kununua madawa kutoka  nje kwa ajili  ya kutibu ugonjwa huo.


Aidha ameitaka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na Halmashauri zote nchini kununua bidhaa hiyo ili kutatua changamoto ya ukosefu wa soko iliyopo kiwandani hapo.


Pamoja na hayo,Mangula amekielekeza kiwanda hicho kujitangaza ndani na nje ya nchi ,ili kuitangaza bidhaa wanayozalisha na kueleza manufaa yake .
Ushauri huo aliotoa  wakati alipotembelea kiwanda hicho  cha Bioteh Products Ltd Kibaha, kabla ya safari yake ya siku kumi nchini Cuba ambako amealikwa na Chama Cha Kikomunist nchini humo.


Mangula alisema gharama zinazotumika kutibu ni kubwa kuliko zinazotumika kuzuia hivyo haina budi kuzuia kabla ya tiba.


Aidha alieleza kuwa  halmashauri zote nchini, MSD pamoja  na Wizara ya Afya zina wajibu wa kushirikiana kununua dawa hizo ili kutatua changamoto ya soko iliyopo.
“Tunahitaji elimu na kujitangaza zaidi juu ya umuhimu wa dawa hii,ili
kuzuia malaria”alisema Mangula.


Hata hivyo ,Mangula alielezea kuwa,kuna viwanda vinne duniani vinavyozalisha dawa ya viuadudu vya mazalia ya mbu ikiwemo Japan ,Marekani ,Cuba na Tanzania hivyo anaamini kinachofanyika Japan ndiokinachofanyika kiwandani hapo .

“Nimepata mwaliko wa kwenda Cuba natarajia kuondoka na mrejesho wa namna kiwanda kinavyoendelea ili niwe na la kujibu kama itatokea kuulizwa lolote juu ya maendeleo ya kiwanda,


“Katika safari hii moja ya eneo nitakalopitia katika safari yangu ni pamoja na kiwanda cha aina hii nchini humo,nimeona itakuwa ni aibu nisije kwenda huko ikatokea kuulizwa lolote nikakosa la kujibu”alisisitiza Mangula.


Mangula alisema, kiwanda kinatakiwa kuzalisha lita mil.sita kwa mwaka, lakini kimeshazalisha lita zaidi ya 400,000 pekee kwa miaka miwili kutokana na kukosa soko la uhakika
“Tunaelezwa viuadudu hivi vinazalishwa na kuwa na uwezo wa kukaa kwa miaka miwili dawa inatakiwa kumwagwa hivyo huwezi kuzalisha kiwango kikubwa wakati soko hakuna “.
Katika hatua nyingine  Mkuu wa Mkoa wa Pwani ,Mhandisi Evarist Ndikilo ,alisema tatizo la soko bado ni tatizo.


Alisema katika Mkoa wa Pwani watu 720,000 waliugua ugonjwa wa malaria ndani ya miaka mitatu iliyopita ambapo vifo vilivyotokana na ugonjwa huo ni 280 hali inayoonyesha ugonjwa huo bado ni tishio kimkoa.


Mhandisi Ndikilo alisema kuwa,Mkoa wa  Pwani unatekeleza agizo la serikali na ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambapo kwasasa ina zaidi ya viwanda 400 vikubwa ,vya kati na vidogo .
Kwa upande wake, meneja wa udhibiti wa ubora na viwango kiwandani hapo , Samwel Mziray , alisema mteja mkuu wa ndani wa bidhaa hiyo ni Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo NDC imeingia mkataba nayo wa kuuza biolarvicides na wizara hiyo kwa mpaka sasa haijaanza kuutumia.


Alitaja changamoto kubwa pia ni madeni kwa halmashauri mbalimbali ambazo zinadaiwa bilioni 1.7 hadi sasa .


Mziray alibainisha kwamba, tatizo jingine ni ucheleweshaji wa malipo kutoka serikalini na soko
Alieleza ,kiwanda bado kina kiasi kidogo cha lita 5,920 zenye gharama ya milioni 78.144.
Kiwanda hicho kiliwekwa jiwe la msingi na Rais mstaafu Jakaya Kikwete oktoba 2013 na kufunguliwa rasmi Julai 2015 ambapo kimegharimu dollar za kimarekani milioni 22 na ajira 110.






Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.