• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Aishukuru Benki ya Stanbic kwa Msaada wa Vifaa Tiba Hospitali ya Tumbi.

Posted on: October 11th, 2025

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Dk. Kusirye Ukio, ameishukuru Benki ya Stanbic Tanzania kwa msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya Shilingi milioni 60, uliotolewa kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani (Tumbi), akisema msaada huo utapunguza changamoto ya upungufu wa vifaa katika utoaji huduma za afya.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano yaliyofanyika hospitalini hapo leo, Oktoba 11, 2025, Dk. Ukio alisema vifaa hivyo vitasaidia kuongeza ufanisi wa huduma na kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi wa afya.

“Tumbi inapokea mamia ya wagonjwa kila siku kutoka mikoa jirani kama Morogoro, Dar es Salaam na Lindi, hivyo msaada huu unaleta ahueni na matumaini mapya kwa wagonjwa na watumishi wetu,” alisema Dk. Ukio.

Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na kompyuta, vitanda, viti vya wagonjwa (wheelchairs), matoroli na vifaa vya usafi, ambavyo vitatumika katika idara mbalimbali zenye wingi wa wagonjwa kila siku.

Msaada huo ulikabidhiwa na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi na Wateja Maalumu wa Stanbic Bank, Omari Ntiga, kwa niaba ya benki hiyo, ambapo alisema kuwa ni sehemu ya mpango wa benki kusaidia jamii kupitia miradi endelevu inayogusa sekta muhimu kama afya, elimu na mazingira.

“Tunatambua sekta ya afya ni uti wa mgongo wa ustawi wa jamii. Tunataka wagonjwa wapate huduma bora na watumishi wafanye kazi katika mazingira bora yenye vifaa vya kisasa,” alisema Ntiga.

Baadhi ya wananchi waliokuwepo wakati wa tukio hilo, akiwemo Kulwa Yohana na Christina Mabawa, walipongeza hatua ya Stanbic Bank, wakisema taasisi binafsi zina nafasi kubwa katika kuboresha huduma za kijamii kupitia ushirikiano na serikali.

“Tunaona si kila kitu lazima kifanywe na Serikali. Msaada kama huu unagusa maisha ya watu moja kwa moja,” alisema Christina.

Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na watumishi wa hospitali, viongozi wa serikali za mitaa na wawakilishi wa Stanbic Bank kutoka matawi mbalimbali ya mkoa wa Pwani.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Wafurahia Mradi wa Shule Mpya ya Sekondari Mwakamo - Ruvu Kibaha.

    October 13, 2025
  • Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Aishukuru Benki ya Stanbic kwa Msaada wa Vifaa Tiba Hospitali ya Tumbi.

    October 11, 2025
  • Katibu Tawala Pwani Ashiriki Maadhimisho ya Miaka 58 ya Hospitali ya Rufaa ya Tumbi.

    October 11, 2025
  • Watendaji wa Vijiji na Mitaa Wapewa Mafunzo ya Mfumo wa iMES kwa Ajili ya Kukusanya Takwimu za Kijinsia Mkoani Pwani.

    October 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.