• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Wananchi Wafurahia Mradi wa Shule Mpya ya Sekondari Mwakamo - Ruvu Kibaha.

Posted on: October 13th, 2025

Wananchi wa Kijiji cha Minazi Mikinda wilayani Kibaha wamefurahia kukamilika kwa ujenzi na usajili wa Shule ya Sekondari Mwakamo-Ruvu, wakisema mradi huo ni mkombozi mkubwa kwa watoto wao na utachangia kuinua elimu pamoja na kuwapatia vijana ujuzi wa kujitegemea.

Wamesema shule hiyo itawaondolea wanafunzi adha ya kutembea umbali mrefu kufuata elimu ya sekondari, sambamba na kuwapa fursa ya kujifunza fursa za ufundi na stadi za maisha, zinazowaandaa kukabiliana na changamoto za ajira.

“Tumeipokea kwa furaha kubwa shule hii. Itasaidia watoto wetu wasome karibu na nyumbani na kupata elimu yenye ujuzi wa kujiajiri,” alisema mmoja wa wananchi, Asha Mkwizu, mkazi wa kijiji hicho.

Ujenzi wa shule hiyo umetekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kupitia Divisheni ya Elimu Sekondari, kwa gharama ya shilingi milioni 528.9 zilizotolewa na Serikali Kuu. Shule hiyo inalenga kutoa elimu ya sekondari yenye mwelekeo wa ujuzi mashinani.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Regina Bieda, amesema mradi huo ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kuinua kiwango cha elimu na kuandaa wanafunzi wenye stadi zinazokidhi mahitaji ya soko la ajira.

“Shule hii ya Mwakamo-Ruvu siyo tu kwamba itarahisisha upatikanaji wa elimu ya sekondari, bali pia itawaandaa wanafunzi wetu kupata ujuzi wa ufundi utakao wawezesha kujitegemea na kuchangia maendeleo ya taifa,” alisema, Bieda.

Kwa upande wake, Afisa Elimu Sekondari wa Wilaya ya Kibaha, Khadija Rajab, amesema shule hiyo inatarajiwa kuanza kupokea wanafunzi mwanzo wa mwaka 2026, na maandalizi ya walimu pamoja na vifaa vya kufundishia yanaendelea.

Mradi huu unatajwa kuwa sehemu ya utekelezaji wa dira ya kitaifa ya elimu bora, jumuishi na yenye mwelekeo wa stadi za maisha, hatua inayotarajiwa kuleta mapinduzi chanya katika elimu ya vijijini na kuchochea maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Wafurahia Mradi wa Shule Mpya ya Sekondari Mwakamo - Ruvu Kibaha.

    October 13, 2025
  • Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Aishukuru Benki ya Stanbic kwa Msaada wa Vifaa Tiba Hospitali ya Tumbi.

    October 11, 2025
  • Katibu Tawala Pwani Ashiriki Maadhimisho ya Miaka 58 ya Hospitali ya Rufaa ya Tumbi.

    October 11, 2025
  • Watendaji wa Vijiji na Mitaa Wapewa Mafunzo ya Mfumo wa iMES kwa Ajili ya Kukusanya Takwimu za Kijinsia Mkoani Pwani.

    October 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.