• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Serikali yatoa ekari 1000 kwa Wakazi wa kisabi

Posted on: March 12th, 2024

Serikali Mkoani Pwani imetoa eneo lenye ukubwa wa ekari 1000 ili lipimwe viwanja na kugawiwa kwa wakazi wanaoishi kwenye eneo oevu kwenye kitongoji cha Kisabi Mlandizi Wilaya ya Kibaha.

Hayo yamebainishwa leo Machi 12, 2024 na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge kwenye mkutano wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Mkuu huyo wa wilaya amefafanua kuwa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira - NEMC lilihadharisha juu ya eneo hilo kutumika kujengwa makazi ya binadamu kwa kuwa ni owevu linaloweza kusababisha madhara yatokanayo na mafuriko kikiwa ni pamoja na uwezekano wa nyumba kutitia.

Kutokana na hali hiyo, ofisi yake iliamua kutafuta eneo rafiki linalofaa kwa makazi ya binadamu ambalo ameeleza kuwa limepatikana katika Kijiji cha Kikongo na sasa maandalizi ya upimaji unaendelea ili wakazi hao wapewe viwanja.

Kwa upande wao, wakazi hao wa Kisabi wameiomba Serikali kuwaacha waendelee kuishi katika eneo hilo ambapo Mkuu wa Wilaya ameahidi kuyafikisha maombi hayo sehemu husika kwa lengo la kutoa maamuzi zaidi ingawa amesisitiza kuwa kutokana na ushauri wa kitaalamu kimazingira, eneo hilo si rafiki kwa makazi hivyo wananchi wanapaswa kuhama.

Katika hatua nyingine, awali, kwenye mkutano uliofanyika Picha ya Ndege Kibaha Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon ameahidi kushughulikia kero ya maji machafu yanayotiririka kutoka kwenye kiwanda cha Keds kilichopo Picha ya Ndege Halmashauri ya mji wa Kibaha.

Kero hiyoa imebainishwa na wakazi wa eneo hilo waliohudhuria kwenye mkutano ulioandaliwa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani ili kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Akizungumza katika mkutano huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Simon amesema Serikali itashughulikia kero hiyo sambamba na kukutana na uongozi wa Kiwanda.

Katika mkutano huo pia Wananchi walieleza kero ya maji kwenye Mtaa wa Lulanzi ambapo Meneja wa Mamlaka ya maji safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salam (DAWASA) Kibaha Alfa Ambokile ameeleza kwamba utekelezaji wa utatuzi wake utaanza hivi karibuni.

Ambokile amesema upo mradi wa maji Pangani unatarajia kuanza utekelezaji wake hivi karibuni mradi ambao utafikisha maji katika eneo hilo la Lulanzi na ilipo Hospitali ya Wilaya.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.