• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Barabara zote ambazo ni ahadi ya Mh. rais Zitekelezwe-RCNdikilo

Posted on: December 23rd, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Pwani mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo amezitaka Taasisi zote za Serikali Mkoani hapo kuandaa na kuratibu ahadi zote zilizotolewa na Viongozi wa Kitaifa na zile zilizo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

"Barabara zote ambazo ni ahadi za Mhe Rais zitekelezwe, sisi tutashirikiana na Chama cha Mapinduzi kuorodhesha ahadi zote na Kumkumbusha katibu wa Rais. Alisema Ndikilo.

Hayo ameeleza wakati wa ufunguzi wa kikao cha Bodi ya barabara ya mkoa pwani ambapo  kabla ya kikao hicho cha  alitembelea baadhi ya Barabara kuona utekelezaji wa Ilani ya CCM na ahadi za Mhe Rais.

Mhe. Ndikilo amesema Mkoa huo unamtandao wa Barabara wa Km 1387.98 zinazo hudumiwa na TANROADS na 5040 zinazo hudumiwa na TARURA. Ameeleza kuwa bajeti ya Barabara ya Mkoa kwa mwaka 2020/21 ni bilioni 35.317 kwa TANROADS na TARURA ni Bilioni 11.245,

"Ukiangalia mtandao wa Barabara na bajeti hizi bado bajeti ni ndogo kulinganiasha na mtandao wa Barabara tulio nao".alisema Ndikilo

Bodi hiyo imeazimia bajeti ya TANROADS na TARURA iwe kwa magawanyo wa asilimia 60 kwa asilimia 40, ili kuwezesha TARURA kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Kupitia kikao hicho cha Bodi ya Barabara Ndikilo ameitaka Mamlaka ya Bandari kuharakisha ujenzi wa Gati eneo la Kilindoni Mafia kwa kuwa tayari kivuko kimekamilika ili kuwezesha magari na abiria kuvushwa kwa usalama, aidha ameitaka Mamlaka hiyo kuchukua ushauri wa Bodi Barabara ya Mkoa ya kujenga Gati kwenye eneo ambalo litatolewa na Halmashauri ya Mafia ambalo halitaathiriwa na Upepo mkali unaosababisha kupwa na kujaa kwa maji.

Kuhusu Daraja la Mkapa Wilayani Rufiji, Bodi hiyo imeshauri TANROADS kufunga Camera ili kuboresha Ulinzi wa daraja Hilo na kubaini watu wanaoweza kuhujumu Taa za Daraja hilo.

Bodi hiyo imeazimia kuwa Viongozi watoe elimu kwa Wananchi wanaodai fidia kupokea malipo yao pale ambapo fedha hizo zinatolewa kwa awamu.

Ndikilo ameitaka TARURA kushirikisha Baraza la Madiwani kuhusu mipango na vipaumbele vya ujenzi wa Barabara kwenye Halmashauri husika.

Ndikilo amewataka Wahe. Wabunge wa Mkoa huo kushiriki vikao hivyo kila wanapohitajika ili kujua hoja na changamoto za Mkoa ili kuzisemea Bungeni na kuwasilisha kwa Wahe. Mawaziri wenye dhamana.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.