• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

CHAMA CHA MSINGI CHA KOROSHO KITAKACHOBAINIKA KUFANYA MCHONGO NA UDANGANYIFU KATIKA MSIMU HUU WA UNUNUZI KITACHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA

Posted on: November 1st, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mhandisi Evarist W. Ndikilo  amesema chama cha msingi cha korosho (AMCOS )ama wataalam wa kupima ubora wa korosho, kitakachobainika kufanya mchongo na udanganyifu katika msimu huu wa ununuzi kitachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufungwa. Aidha amewasihi Wakuu wa Wilaya zote Mkoani Pwani, kusimamia na kuweka mazingira wezeshi ili msimu uwe na mafanikio makubwa. Hata hivyo, amemtaka Katibu Tawala Msaidizi - Uchumi na uzalishaji Mkoani Pwani, Bw. Shangwe Twamala kusimamia mnada wa ununuzi wa korosho unaoanza rasmi Novemba 8 mwaka 2017 Mkoani Pwani kwa uwazi ili kuondoa malalamiko.

Akifunga kikao cha tathmini na maandalizi ya msimu mpya wa zao hilo la kibiashara, Mwenyekiti wa kikao hicho, Mhandisi Ndikilo, alisema hatokubali mnada huo kugeuzwa kuwa ni dili. Aliziasa AMCOS na wataalamu wa kupima ubora kuepukana na na udanganyifu kwenye ubora wa korosho. “Kumekuwepo na udanganyifu mkubwa unaofanyika katika maghala ya kuhifadhia korosho ambapo baadhi za AMCOS zimebainika kusababisha uzito wa korosho zilizopimwa kwenye maghala, Ambapo kabla ya mnada hupungua kwa kiasi kikubwa wakati mnunuzi anapokabidhiwa korosho hizo” alielezea.

Mhe. Ndikilo alieleza kuwa, Wilaya ya Mafia ina tani 200 za korosho na katika mnada wa Novemba 8 kutakuwa na tani 50 kutoka wilaya hiyo. Mkoa wa Lindi na Mtwara mnada umeshaanza hivyo hataki kusikia kisingizio katika mnada huo. Katika hatua nyingine, aliitaka bodi ya korosho kupeleka magunia Mkoani hapo, kwani yaliyopo hayatoshi na kusababisha athari kwa wakulima na kuhofia kukosa faida.

Mhandisi Ndikilo alisema, kutaimarishwa vizuia vya kudhibiti utoroshwaji wa korosho nje ya Wilaya na Mkoa . Alikemea biashara ya korosho kufanywa katika mfumo wa kangomba ambao huwakandamiza wakulima wa zao hilo. Mhandisi Ndikilo, alisema korosho zote zitakazokutwa kwenye magari yatakayokamatwa yakiwa kwenye mifumo isiyo rasmi badala ya stakabadhi ghalani ambao unatambulika, korosho hizo zitataifishwa  na mtuhumiwa atakamatwa na Jeshi la Polisi.

Mkuu wa wilaya ya Mkuranga, Mhe. Filberto Sanga alisema zao la korosho ni zao la biashara ambalo linanufaisha mkulima na taifa kwa ujumla. Alisema kutokana na umuhimu huo halipaswi kufanyiwa ujanjaujanja kwa watu kujinufaisha zaidi ya mkulima husika.  Mhe. Sanga alieleza kwamba, korosho za baadhi ya wakulima zipo chini kwenye maji zinaharibika kwa kukosa magunia ya kuzihifadhi. Nae mwenyekiti wa CORECU Mkoani Pwani, Bw. Rajabu Ng’onoma alisema awali waliagiza magunia ya ziada ambayo waliyahifadhi kwenye ghala lao la CORECU.“Tulijua yatatosheleza na yanaweza kutumika na kubaki lakini hapo kipindi cha kati ilitokea tatizo juu ya magunia hayo ambapo wanaodaiwa kuhusika wameshakamatwa na kwasasa wanauachia mhimili lengwa uchukue mkondo wake ” alifafanua Ng’onoma . Bw. Ng’onoma alisema wanatekeleza majukumu yao kwa uzalendo na uchungu ili kuhakikisha korosho inaleta mapinduzi makubwa na maendeleo chanya Kimkoa

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.