• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Geraruma ahimiza Usimamizi wa Fedha za Umma

Posted on: May 1st, 2022

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahil Geraruma amewaasa viongozi, watendaji na wataalamu wa Halmashauri kusimamia fedha za miradi na kujenga tabia ya kuhifadhi nyaraka za ujenzi wa miradi ya maendeleo ili kujiepusha na mkanganyiko wakati wa ukaguzi.

Akikagua miradi ya maendeleo Leo Mei 1, 2022 katika mradi wa Zahanati ya Nyanda Katundu na barabara ya Mji Utete, wilayani Rufiji Mkoani Pwani, Guraruma aliwaasa watendaji hao kufuatilia miradi ya maendeleo kwa maslahi mapana ya wananchi kwenye Maeneo Yao.

Alihimiza kuwa Watumishi wanapaswa kutekeleza miradi kwa uadilifu na kuzingatia usimamizi wa miradi kwa maslahi mapana ya wananchi.

Pia Guraruma alikemea baadhi ya watumishi na viongozi nchini kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani wanasababisha kudorora kwa miradi.

Akikagua mradi wa vijana kikundi cha Kumekucha Umwe Kaskazini, alielekeza Halmashauri kutenga fedha za vijana na kuhakikisha vikundi vinarejesha mikopo kwa wakati lengwa.

Kuhusu suala la Sensa, Bw. Geraruma amehimiza wananchi kujitokeza katika Zoezi hilo Mwezi Agosti mwaka huu kwa Ajili ya mipango ya maendeleo pasipo kupuuzia.

Nae Mkurugenzi wa Halmashauri ya Rufiji,John Kayombo alisema, zahanati hiyo imepewa milioni 50 ambapo imebaki zaidi ya milioni Saba na ujenzi utaendelea.

Awali, akipokea mwenge wa Uhuru kutoka Mkoani Lindi, mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge, aliweka bayana kwamba jumla ya nyumba 515,668 zimeingizwa kwenye mfumo wa Zoezi la anwani za makazi sawa na asilimia 105.61.

Alisema kufuatia maandalizi ya sensa na makazi wamejipanga na kuendelea kuhimiza wananchi kujitokeza kwenye Zoezi hilo agost mwaka huu.

"Mkoa wetu ulikuwa miongoni mwa mikoa 13 kwenye zoezi la sensa ya majaribio na Tunashukuru limefanya vizuri "Kunenge alisema.

Mkuu huyo wa mkoa alieleza kuwa,kiasi cha sh.milioni 816 .2 kutoka Serikali Kuu kimepokelewa na Halmashauri zimechangia milioni 320.

Pamoja na hayo, Kunenge alieleza mwenge wa uhuru ukiwa Mkoani hapo utapitia miradi 111 yenye gharama ya Zaidi ya Bilioni 69.2.

"Kati ya miradi hiyo miradi 25 itawekwa mawe ya msingi, 22 itazinduliwa, 6 itafunguliwa na 58 kukaguliwa"alifafanua Kunenge.

Akipokea mwenge wa uhuru Mkuu wa wilaya ya Rufiji Edward Gowelle kutoka kwa Mkuu wa mkoa,alisema mwenge ukiwa Rufiji utapitia miradi sita yenye thamani ya milioni 6.5.

Kati ya miradi iliyotembelewa Rufiji ni pamoja na Zahanati Nyanda Katundu, barabara Mji Utete, mradi wa vijana kikundi cha Kumekucha Umwe Kaskazini, Mradi wa Uraghibishaji falsafa ya mwenge,ghala la mwananchi na madarasa ya Sekondari Mkongo.

Mwenge wa uhuru Mei 2 unatarajiwa kupokelewa huko Mkupuka wilaya ya Kibiti.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.