• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Hakikisheni Miradi ya Barabara mnayoisimamia inaisha kwa wakati-RC Ndikilo

Posted on: December 15th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo amemtaka Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini Tanzania (TARURA) Mkoa wa Pwani kuhakikisha Miradi ya Barabara wanayoisimamia Mkoani Hapo inakamilika kwa wakati.

Ndikilo aliyasema hayo leo Desemba 15,2020 wakati alipofanya ziara kukagua baadhi ya Miradi ya Barabara kwenye Wilaya za Kibaha na Bagamoyo.

katika ziara hiyo Ndikilo amekagua Ujenzi wa Barabara ya TAMCO -Mapinga yenye urefu wa Kilometa 23, akiwa katika Mradi huo Ndikilo amemtaka Meneja wa TANROADS kusimamia Mkandarasi aliyepatikana kuanza ujenzi kipande cha Mita 600 kwa haraka. Barabara hiyo inajengwa kwa awamu hadi sasa zimejengwa Kilometa 2.9 kwa kiwango cha lami na kubaki Kilometa 20.1. Aidha, Amemtaka Mratibu wa TARURA Mkoani hapo kuandaa mpango wa Kujenga barabara ya mzunguko (Roundabout) kwa kiwango cha changarawe katika makutano ya barabara za NIDA -Loliondo Mjini Kibaha na kuwasilisha mpango huo siku ya kikao cha Bodi ya Barabara tarehe 22 Desemba 2020, Ndikilo amefikia uamuzi huo baada ya TARURA kueleza kuwa hawana fedha kiasi cha shilingi Milioni 400 za kujenga roundabout hiyo kwa sasa hadi Julai 2021." Hatuwezi kukaa zaidi ya mwaka mmoja na kupaacha eneo hili bila matengenezo, hapa ni katikati ya Mji tuje na mpango wa kuparekebisha kwanza kwa kiwango cha changarawe kabla ya kupata fedha hizo" alisema Ndikilo.

"Barabara ya TAMCO- Mapinga ni ahadi ya Mhe Rais wakati wa Kampeni alipokuja Mkoani kwetu na ipo kwenye Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndani ya Kipindi cha miaka 5 tunauhakika Barabara hii itakamilika kujengwa kwa kiwango cha lami, Barabara hii ni ya muhimu kwa kuwa eneo hili lina ardhi kwa ajili ya Ujenzi wa Viwanda ikikamilika itavutia wawekezaji, ni njia rahisi ya kuunganisha Makao Makuu ya Mkoa Kibaha na Wilaya ya Bagamoyo" ameeleza Ndikilo. Amesema kuwa Ujenzi wa Barabara hiyo utapelekea kuwepo kwa usafiri wa uhakika na hivyo kusaidia Wanafunzi na jamii ya kuondokana kero ya kutembea umbali mrefu.

Akiwa kwenye Barabara ya kuelekea kwenye eneo la Viwanda la Zegereni (Visiga -Zegereni) Kibaha yenye urefu wa kilometa 12 ameeleza kuwa barabara hiyo inaharibika mara kwa mara wakati wa mvua. "Wenye viwanda wamekuwa wakilalamika kuwa wanashindwa kutoa bidhaa viwandani kwenda sokoni ambapo kuna viwanda vikubwa 25 Vinavyofanya kazi kwenye eneo hilo, kwa kuwa serikali inahimiza ujenzi wa viwanda na wadau wameitikia wito wa ujenzi wa viwanda lazima tuhakikishe tunawawekea mazingira mazuri kwa kujenga barabara ili zipitike na kuwaondolea kero ya kusafirisha bidhaa na malighafi kwenda viwandani na sokoni,”alisema Ndikilo.

"Mpango wa Serikali ya Mkoa ni kuhakikisha barabara hii inapitika mwaka mzima ili wenye viwanda wanaposafirisha malighafi kwenda viwandani na kutoa bidhaa kupeleka sokoni wasafirishe kwa muda mfupi" nimemuona mkandarasi yupo eneo la mradi anatengeneza maeneo korofi, habari njema ni kwamba Serikali pia imetoa fedha shilingi bilioni 1.2 kwa ajili ya ujenzi wa kilometa moja ya lami ya barabara hii" alisema Ndikilo.

Akikagua Barabara ya Kwa Mathias, Nyumbu Msangani (Kibaha) yenye Urefu wa Km 8.5, amewathibitishia Vikosi vya Jeshi Kamandi ya Nchi kavu, Shirika la Nyumbu na wananchi wa eneo hilo kuwa wanaendelea kujenga kwa awamu hadi kukamilisha kilometa zote 8.5. "Niwapongeze TANROADS kwa kujenga Km 2.32 kwa kiwango cha lami kwani kabla ya ujenzi huo magari na usafiri ulikuwa mgumu eneo hili" kwa sasa TANROADS tayari wamepata mkandarasi na wataanza ujenzi wa M 600 hadi geti la Shirika la Nyumbu. " nimeridhika na kiwango kilichojengwa rai yangu ni kwa mkandarasi anyaejenga hizi M 600 kufanya haraka na kukamilisha ndani ya miezi 8 iliyopangwa.

Akikagua Ujenzi wa barabara Eneo Korofi la Vigwaza, amepongeza Ujenzi huo na kusema kuwa Uboreshaji wa maeneo korofi utasaidia kuepusha ajali kutokea na kuboresha usalama na hali ya barabara,"Barabara ya Morogoro ni ya Muhimu sana inasafirisha abiria na mizigo kwenda mikoani na Nchi jirani, mara nyingi pamekuwa pakiharibika na kusababisha msongamano, nimefurahi kusikia baada ya siku is mbili mtafungua magari yataanza kupita hapa Vigwaza kazi you ni nzuri" alisema Ndikilo.

Ndikilo ametembelea pia ujenzi wa Barabara ya Vigwaza-Bandari kavu ya Kwala yenye to urefu wa km 15.5 inayojengwa kwa kiwango cha zege, amepongeza ujenzi huo unaogharimu bilioni 30 na half kumtaka Mkandarasi kufanya is kazi is usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi huo, amezitaka Mamlaka ya Bandari TPA kuhakikisha inawalipa fidia wananchi waliopisha mradi huo you ifikapo Januari 15, 2020. Amewataka wawekezaji kuchangamkia fursa ya ujenzi wa Viwanda na uwekezaji mwingine kwenye eneo hilo.


Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.