• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Hakikisheni Ujenzi huu unakamilika Haraka:RC Ndikilo

Posted on: February 17th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo, amemtaka Mkandarasi wa ujenzi wa mradi wa Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya Kibiti kuhakikisha  ujenzi huo unakwenda na unakamilika  haraka.

Aliyasema hayo Wilayani Kibiti wakati wa ziara yake Wilayani humo, ambopo alitembelea  na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mhandisi Ndikilo alisema kuwa ,Mkandarasi suma JKT anapaswa kuhakikisha ujenzi  unakamilika kwa wakati ili utoaji wahuduma uweze kuimarika, kwani kwa sasa huduma zinatolewa katika mazingira magumu na gharama kubwaa kutoka  na Ofisi kupanga kwenye majengo ya watu binafsi.

“Hakikisheni Jengo hili linakamilika kwa wakati kwani litafanya Halmashauri kutoa huduma bora kwa wananchi  pia huduma zitatolewa sehemu moja , tofauti na sasa” alisema Mhandisi Ndikilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Gulamuhussein Kifu alisema kuwa ujenzi unaendelea na thamani ya ujenzi hadi kukamilika itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 5.3.

Kifu alisema kuwa,Ujenzi huo ambao unafanywa na Suma JKT unaendelea vizuri kwa sasa tayari  ujenzi wa majengo ya chini umekamilika na wanatarajia kuweka zege kwa ajili ya kuanza Ghorofa ya kwanza.

“Tunaishukuru sana Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dk John Magufuli, kwa kupata fedha  kwa ajili ya ujenzi huu na utakapokamilika utaondoa  adha ya Halmashauri kupanga kwenye majengo ya mtu binafsi “ alisema Kifu.

Alisema kuwa, Ofisi yake na baadhi ya Ofisi ziko kwenye jengo la Idara ya Maji , Ofisi ya Mkurugenzi na baadhi ya Idara wamebanana kwenye jengo la mtu binafsi huku Ofisi nyingine zikiwa sehemu mbalimbali.

“Tutahakikisha ujenzi huu unakamilika kwa wakati ili tuanze kutumia majengo yetu badala ya kupanga mitaani ambako si salama sana , tofauti na kuwa na Ofisi yetu ambayo itarahisisha utendaji kazi tofauti na ilivyo sasa”alisema kifu.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya hiyo Alvera Ndabagoye alisema kuwa hadi sasa wameshampatia mkandarasi kiasi cha shilingi milioni 961.

Ndabagoye alisema kuwa fedha zilizopo benki ni shilingi Bilioni tatu kwa ajili ya ujenzi huo wa Makao makuu ya Halmashauri, hivyo hakuna tatizo la fedha.

Naye kwa upande wake Msimamizi wa ujenzi huo kutoka Suma JKT Eric Mtayoba alisema kuwa ujenzi ulichelewa kutokana na ukosefu wa umeme, maji ,na barabara ambapo kwa sasa changamoto hizo hazipo tena na wanatarajia kukamilisha ujenzi huo mwanzoni mwa mwaka ujao.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.