• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Hoteli ya The Maybom kunafaisha wananchi wa Mkoa Pwani kwa kutoa ajira na huduma mbalimbali za Kijamii.

Posted on: September 6th, 2025

Wananchi wa Mkoa wa Pwani watanufaika na ajira na huduma mbalimbali za kijamii baada ya kuzinduliwa kwa hoteli mpya ya The Mayborn iliyopo Mtaa wa Lulanzi, Kata ya Picha ya Ndege katika Manispaa ya Kibaha.

Hoteli hiyo, iliyofunguliwa rasmi Septemba 4, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge, inatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi kwa wakazi wa eneo hilo na mkoa mzima.

Mkurugenzi Mtendaji wa hoteli hiyo, Fikirini Mushi, alisema ujenzi wa hoteli hiyo ulianza mwaka 2010 baada ya kununua ardhi mwaka 2009, ukidhaminiwa na Benki ya Biashara ya NBC. Alieleza kuwa lengo kuu la uwekezaji huo ni kuleta huduma za kiwango cha juu karibu na wananchi, badala ya wao kulazimika kusafiri Dar es Salaam.

“Huduma zitakazopatikana hapa ni pamoja na malazi ya kisasa, kumbi za mikutano na harusi, pamoja na maeneo ya biashara ambayo yatapunguza gharama na muda wa wananchi kufuata huduma hizo mbali,” alisema Mushi.

Akaongeza kuwa hoteli hiyo itafungua fursa za ajira kwa wakazi wa Kibaha na maeneo jirani, kukuza mapato ya Halmashauri kupitia kodi, na kuhamasisha wawekezaji wengine kuwekeza Pwani.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge alisema Serikali inaunga mkono uwekezaji huo na kueleza kuwa ni sehemu ya mpango wa kukuza uchumi wa mkoa huo kwa kuhakikisha wananchi wananufaika moja kwa moja.

“Uwepo wa hoteli hii unasaidia kuondoa changamoto ya wawekezaji kulazimika kuishi Dar es Salaam. Sasa wanapata huduma kwa ukaribu na kwa hadhi ya Manispaa ya Kibaha,” alisema Kunenge.

Hata hivyo, Mushi alitaja changamoto ya miundombinu ya barabara, hasa nyakati za mvua, lakini akaeleza kuwa ana imani Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji.

Hoteli ya The Mayborn inatazamwa kuwa kichocheo cha maendeleo ya sekta ya huduma, ajira na biashara katika Mkoa wa Pwani.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Pwani Yatenga Maeneo 27 ya Kongani Kukuza Uwekezaji na Viwanda.

    September 11, 2025
  • Lishe Bora Chachu ya Maendeleo - RC Pwani.

    September 09, 2025
  • Pwani Kunufaika na Vyandarua Milioni 1.2 Kukabili Malaria.

    September 09, 2025
  • Timu ya Michezo ya Watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani yashiriki Uzinduzi wa Mashindano ya 39 ya SHIMIWI.

    September 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.