• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Idadi wasiojya kusoma ,kuandika Kuhesabu yapungua nchini

Posted on: October 12th, 2023

Idadi ya watu wazima wanaojua kusoma, kuandika na kuhesabu nchini imepungua kutokana na Serikali kuanzisha program mbalimbali kuliwezesha kundi hilo kupata maarifa.

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa Kongamano la kitaifa la Maadhimisho ya Juma la Elimu kwa watu wazima, Dkt. Sempeo Siafu linalofanyika kitaifa mkoani Pwani.

Amesema, kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni - UNESCO, idadi ya watu wanaojua kusoma, kuandika na kuhesabu imepungua tangu nchi ya Tanzania ipate uhuru, kutokana na hali hiyo Wizara ya Elimu ilianzisha program maalum kwa ajili ya kuwasaidia watu wazima na vijana waliositisha masomo kurudi shule.

“Hayati baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alianzisha kampeni mbalimbali zinazohamasisha wananchi kujua kusoma na kuandika, na ukiangalia tulikotoka na sasa tumerudi nyuma, natoa rai kuweka mikakati ya pamoja ili kuondoa changamoto hii nchini, taifa la watu walioelimika ni rahisi kuleta maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla,” amesema Dkt. Siafu.

Ameeleza kuwa, program ya Elimu ya awali itaendelea kufanya vizuri endapo watu wazima watajua kusoma na kuandika kwa ajili ya ushirikiano baina yao na walimu katika kufuatilia maendeleo ya watoto shuleni.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Elimu Msingi, Josephat Luoga amesema, Serikali imekuwa ikitekeleza program mbalimbali za elimu ya watu wazima ili kuongeza idadi ya watu wanaojua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Amezitaja program hizo kuwa ni Mpango wa Elimu Msingi kwa walioikosa MEMKWA, Mpango wa Elimu Sekondari kwa njia mbadala, Mpango wa Elimu changamani walio nje ya shule, uzalishaji mali, shughuli za ugani na vikundi vya kuweka na kukopa - VICOBA.

Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Watu Wazima, Elimu Maalum na Michezo kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI, Ernest Hinju amesema wanao mtandao wa kutosha kuhakikisha kila mtu mzima mwenye lengo la kusoma atapata elimu hiyo katika eneo lake.

Afisa Elimu mkoa wa Pwani, Sarah Mlaki amesema mkoa huo unatekeleza programu mbalimbali kwa halmashauri zote kama vile Mpango wa Elimu ya Msingi kwa waliokosa - MEMKWA, jumla ya wanafunzi 1943 wakiwemo wavulana 1117 na wasichana 826 wamenufaika nao.

Ameongeza kuwa mkoa huo, unatekeleza program ya Mpango wa Uwiano kati ya Elimu ya watu wazima na Jamii - MUKAJE yenye jumla ya wanafunzi 2080 ikitajwa kuwa program nzuri ya elimu nje ya mfumo rasmi kwani wanajifunza na shughuli za uzalishaji mali kama vile mapishi, ushonaji, mapambo, ufumaji, ususi na usindikaji.

Baadhi ya wanufaika wa programu ya Elimu ya watu wazima akiwemo Siri Kibinde amesema kwa sasa amejua kusoma na kufanya shughuli za ujasiriamali kama vile ushonaji, mapambo, ususi na usindikaji.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.