• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Aongoza Ufunguzi wa Kikao cha Mpango wa MTAKUWWA II.

Posted on: July 18th, 2025

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Nsajigwa George, leo Julai 18, 2025, ameongoza ufunguzi rasmi wa kikao cha kwanza cha Kamati ya Mpango Kazi wa Pili wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA II) kwa mwaka 2024/2025 hadi 2028/2029. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Kibaha.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Nsajigwa ametoa wito kwa wadau wote kushirikiana kikamilifu na Serikali katika utekelezaji wa mpango huo kwa kuhakikisha kuwa Kamati za MTAKUWWA zinaanzishwa na kuimarishwa kuanzia ngazi ya kijiji/mtaa hadi taifa.

Nsajigwa alibainisha kuwa utekelezaji wa Mpango wa Kwanza (MTAKUWWA I) umeleta mafanikio makubwa, ikiwemo kupungua kwa matukio ya ukatili wa kimwili kwa wanawake kutoka asilimia 40 mwaka 2015 hadi asilimia 27 mwaka 2022, ukatili wa kingono kutoka asilimia 17 hadi 12, na visa vya ukeketaji kutoka asilimia 10 hadi 8.

“Mafanikio haya yametokana na juhudi za pamoja kati ya Serikali na wadau mbalimbali, kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, pamoja na OR-TAMISEMI,” alisema Nsajigwa.

Aidha, alieleza kuwa Serikali imeongeza huduma za mikopo yenye masharti nafuu kupitia mifuko mbalimbali, ikiwemo asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Lengo ni kuwawezesha kiuchumi ili kupunguza ukatili unaochochewa na hali ngumu ya maisha.

Katika kipindi cha MTAKUWWA I, jumla ya Kamati 18,186 za Ulinzi wa Wanawake na Watoto ziliundwa nchi nzima, huku Mkoa wa Pwani ukiunda Kamati 756 sawa na asilimia 93.5 ya lengo.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Dkt. Kusirye Ukio, alisisitiza umuhimu wa ulinzi wa mama na mtoto akisema, “Kumlinda mama ni kupunguza asilimia 75 ya matatizo ya mtoto.” Aliongeza kuwa maboresho ya miundombinu ya afya yamechangia utoaji wa huduma bora kwa waathirika wa ukatili na kusaidia kubadilisha mitazamo hasi katika jamii.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Pwani, Bi. Grace Tete, akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mikopo ya asilimia 10, alisisitiza umuhimu wa wanufaika kubuni biashara zenye tija zinazokidhi mahitaji ya soko ili kujitegemea kiuchumi na kufungua fursa zaidi za kifedha.

Mpango huu wa Pili wa Taifa (MTAKUWWA II) ni mwendelezo wa jitihada za kitaifa kuhakikisha wanawake na watoto wanalindwa, wanathaminiwa na kuwekewa mazingira salama ya kuishi na kuendeleza maisha yao kwa ushirikiano wa jamii nzima.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Aongoza Ufunguzi wa Kikao cha Mpango wa MTAKUWWA II.

    July 18, 2025
  • Utekelezaji TIRP2 wa TRC unamanufaa kwa jamii - Nsajigwa.

    July 17, 2025
  • Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Aongoza Kikao Kazi cha Viongozi, Asisitiza Uboreshaji wa Vyanzo vya Mapato.

    July 15, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Pwani Akutana na Ujumbe wa NBC Kujadili Ushirikiano wa Kimaendeleo.

    July 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.