• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kero za Wanafunzi kutemmea Umbali Mrefu yatatuliwa Mkuranga

Posted on: November 9th, 2023

Serikali imetatua kero ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata elimu ya Sekondari kutoka Kijiji cha Kilimahewa kwenda Kiimbwanindi wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani.

Hayo yamebainika Mkuranga leo Novemba 8, 2023, katika muendelezo wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge anayetembelea na kukagua miradi ya maendeleo Mkoani humo.

Kutokana na kero hiyo iliyodumu kwa muda mrefu, Serikali ilianza ujenzi wa shule ya Sekondari ya kutwa Kilimahewa ili kuondoa kadhia hiyo.

Taarifa ya utekelezaji mradi huo inaeleza kuwa ujenzi huo kwa sasa umefikia asilimia 92 na kuwa unatarajiwa kukamilika wakati wowote mwezi huu na kugharimu kiasi cha sh. milioni 528.9.

"Mmemtendea haki Mhe. Rais, mmetuheshimisha kukamilisha ujenzi huu, ni shule bora miongoni mwa shule zilizo bora," alieleza Kunenge.

Awali mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Hadija Nasir alieleza kuwa kukamilika kwa mradi huo kutawezesha zoezi la ufundishaji na kujifunza kukamilika kiufasaha kutokana na miundombinu hiyo.

"Tunaishukuru Serikali kutuletea fedha nyingi hapa Mkuranga, awali watoto walikuwa wakitembea masafa marefu ili kufika Mkamba Sekondari, uwepo wa shule hii sasa unaondoa adha hiyo na tunashukuru inaenda kukamilika kwani tumefikia asilimia 80 ya utekelezaji," amesema DC Hadija na akaahidi kufanya usimamizi ili ujenzi huo ukamilike ndani ya wiki mbili.

Awali, akitoa taarifa ya mradi wa shule hiyo, Kaimu Mkuu wa shule ya Sekondari ya kutwa Kilimahewa, Rabii Athumani alifafanua kuwa, shule ilianza machi 2023 baada ya kupata usajili.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amekagua ujenzi wa shule ya Sekondari Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyopo Shungubweni, ambao utagharimu shilingi milioni 595.

Akiwa Mkuranga Mkuu huyo wa Mkoa ametembelea pia kiwanda cha kubangua korosho kata ya Kiparanganda (Sabayi Agroprocessing Ltd. na akakagua ujenzi wa barabara inayojengwa kwa kiwango cha lami yenye urefu wa km.0.5 pamoja na kuzungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.