• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kikwete awaasa wenye Viwanda Mkoani Pwani na nchini kuzalisha bidhaa zora zinazolingana na Soko la ushindani katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Posted on: October 6th, 2022

Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt.Jakaya Kikwete amewaasa wenye viwanda Mkoani Pwani na nchi kijumla kuzalisha bidhaa bora zinazolingana na soko la ushindani katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kujiinua kimasoko.

Aidha ameutaka mkoa huo kuboresha Mazingira ya Uwekezaji na kusimamia maeneo yanayotengwa kwa ajili ya uwekezaji (kongani) kwa kuzingatia maendeleo yanavyokuwa kwa maslahi ya vizazi vijavyo.

Akifungua maonyesho ya tatu ya wiki ya biashara na uwekezaji Mkoani Pwani yanayofanyika Mailmoja Kibaha Mjini,Kikwete alieleza Tanzania ni miongoni mwa nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika mashariki ambapo zipo nchi saba hivyo Kuna kila sababu ya kuzalisha bidhaa zenye viwango na ubora .

"Hatua tuliyofikia tupo katika ushindani Lazima tuzalishe bidhaa zetu na kuwa bora ,nchi yetu imesaini Africa Continental free trade area ,biashara huru Afrika ,mtakuja kusema Serikali izue bidhaa zinazojiuza Lakini tutashindwa kwakuwa mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki itafungua "

"Tuhakikishe tunazalisha bidhaa Bora vinginevyo itakula kwetu,hata kama tunazalisha kibongobonho lakini hao wabongo wanataka bidhaa bora pia"alisisitiza Kikwete.

Hata hivyo Kikwete alisema ,Uchumi unakuwa kwa uwekezaji Kama hakuna uwekezaji hakuna uchumi na utakwama na kusinyaa.

Vilevile aliwashauri kusimamia Maeneo wanayojenga viwanda ,kwani vipo viwanda vilivyojengwa wilayani Mkuranga ambavyo vipo barabarani kulingana na mahitaji na maendeleo yanavyokuwa vinaweza kuja kumegwa kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya barabara.

Kikwete alimpongeza mkuu wa mkoa wa Pwani alhaj Abubakari Kunenge kwa kutenga maeneo ya uwekezaji,kongani za viwanda.

Katika hatua nyingine Kikwete alisema Serikali inafanya kazi nzuri,katika kuinua sekta ya uwekezaji na viwanda na kuimarisha Mazingira bora ya uwekezaji.

"Tumeona Mamlaka ya maji safi na maji taka (DAWASA) wanavyoweka nguvu kubwa ya kuboresha miundombinu ya maji safi na salama na kufikisha kwenye maeneo ya uwekezaji , Serikali imejenga reli ya kisasa (SGR), imeongeza huduma za usafiri wa anga na vingine vimejengwa na kujenga kongani za viwanda."

Alisema uwekezaji una manufaa makubwa katika kutoa ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja ,ambapo itasaidia vijana kupata ajira na kuondokana na kushinda kucheza pool.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Pwani Mhe Abubakari Kunenge alieleza mkoa una viwanda 1,460 kati ya hivyo 90 ni vikubwa.

Alieleza kwamba ,mkoa huo imejipanga katika sera ya uwekezaji na viwanda kwa kutekeleza kwa vitendo .

"Ukitaka kuwekeza njoo Mkoani Pwani,tumejipanga kwa kuweka Mazingira Bora na ulinzi na Usalama ,tumeboresha miundombinu ya barabara,maji,umeme kwa ajili ya viwanda"

"Pia kwa kuzingatia masuala ya uwekezaji na changamoto zao mkoa tumetenga kila siku ya Jumanne tuna Taasisi 19 ambazo zinasikiliza kero za wawekezaji na kuzitafutia ufumbuzi"alisema Kunenge.

RC Kunenge alielezea Kuwa ,katika uwekezaji wamesheheni kwenye nyanja zote ikiwemo kilimo, biashara, ufugaji,uchumi wa blue (utalii) Kuna fukwe yenye km.1,132 kwa ajili ya uwekezaji,Kuna saadan, selou iliyopo Rufiji ambapo mkoa una jumlanya vivutio 72.

Akifafanua zaidi Kunenge alisema ,upande wa maji kwa wawekezaji na kusambaza maji kwa jamii RUWASA na DAWASA mkoa zinafikisha maji kwa asilimia 86.

Anasema Serikali ilipeleka Bilioni 197 kwa Ruwasa na DAWASA kwa ajili ya kuhakikisha inasogeza huduma ya maji ndani ya mkoa na hatua mbalimbali za zinaendelea huku miradi mingine ikiwa imekamilishwa.

Alitoa rai kwa Watanzania kupenda na kuvienzi viwanda vidogo vidogo lakini pia kununua bidhaa zinazozalishwa katika viwanda hivyo ili kuviwezesha viweze kupiga hatua zaidi.

Maonyesho ya tatu ya wiki ya biashara na uwekezaji Mkoani Pwani,yalianza mwaka 2018 akiwa mkuu wa mkoa wakati huo Evarist Ndikilo ,na haya ya Sasa ni Mara ya tatu ambapo yameandaliwa na mkoa kwa kushirikiana na SIDO ,kuratibiwa na Tantrade na wafadhili wakuu ni SINOTAN.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.