• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kiwanda Kikubwa cha Kuchakata Mihogo chajengwa Pwani

Posted on: April 15th, 2021

Serikali Mkoani Pwani kwa kushirikiana  na wadau mbali mbali wa zao la Mhogo wameazimia kwa pamoja kujenga ujenzi wa kiwanda kikubwa kwa ajili ya kuchakata zao la Muhugo ambacho kitajengwa katika eneo la Chailinze lililopo  halmashaurli ya Chalinze Wilayani Bagamoyo kwa lengo la kuwakomboa  wakulima  wa  zao  hilo ili  kuondokana na chanagamoto zinazowakabili katika upatikaniji soko.

Maazimio hayo ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata zao  hilo la Muhogo   yamefanyika katika mkutano wa wadau wa zao la muhogo katika Mkoa wa Pwani ambacho kimeweza kuwajumuisha viongozi mbali mbali wa serikali pamoja na wadau wa zao hilo wakiwemo wakulima kwa lengo la kuweka mikakati na kujadili  changamoto  zinazowakabili wakulima hao wa zao la muhugo.

Akizungumza  katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo   alisema kwamba  lengo   kubwa serikali ni kuweka mikakati madhubuti ambayo itawasaidia kuwakomboa wakulima  wa zao la muhogo hivyo ujenzi  wa kiwanda hicho utakuwa ni mkombozi mkubwa na chachu ya kuleta  mabadiliko chanya ya kimaendeleo.

Aidha, Ndikilo amewataka maofisa ugani waliopo Mkoani humo kujenga tabia ya kuwatembelea wakulima wa zao la muhogo ili waweze kutoa elimu ya namna ya uzalishaji wa zao hilo.

Alisema ,zao la Muhogo ni moja ya zao muhimu na kwamba likitumika vizuri linaweza kuwaongezea wakulima kipato na hata kuongeza kipato cha Mkoa na hata kujenga uchumi wa Taifa.

Ndikilo ,alisema kuwa wakulima wengi wanalima zao hilo huku wakiwa hawana utaalamu wala elimu ya kutosha juu ya zao hilo na kwamba ni wakati wa maafisa ugani kuona namna ya kuwatembelea wakulima kwa kuwapa elimu ya zao hilo.

Aliongeza kuwa,mkoa wa Pwani unajumla ya hekta 3,353,900 ambapo eneo linalofaa kwa kilimo ni hekta 1,933,224 sawa na asilimia 57.66 ya eneo lote.

Alisema, pamoja na kuwepo kwa ukubwa wa eneo hilo lakini bado Muhogo hulimwa kwa kiasi kidogo ikiwa ni wastani wa hekta 60,703 na kuzalisha tani 500,000 hadi 650,000 kwa mwaka huku akisema eneo hilo ni asilimia tatu.

" Kwa upande wa tija nayo ipo chini kwa miaka mitano iliyopita uzalishaji kwa eneo ni wastani wa tani 6.5 hadi 7.6 kwa hekta ingawa yapo maeneo machache hasa Kibiti na Rufiji ambako tija ni kati ya tani 9 hadi 18 kwa hekta wakati tija inayopendekezwa kitaalamu kuwa ni tani 20 kwa hekta" alisema Ndikilo.

Kuhsu usindikaji mkuu huyo wa mkoa alisema mkoa bado haufanyi vizuri pamoja na kuwepo kwa juhudi za kuanzisha vikundi na Viwanda vya usindikaji kwani vikundi 32 vilivyopo katika Mkoa huo havisindiki mihogo kwa madai ya kukosa soko la uhakika.

Mwenyekiti wa Chama Cha Wadau wa Zao la Muhogo (TACAPPA) Mwantumu Mahiza, alisema endapo wakulima watahamasishwa kuhusiana na zao hilo litawasaidia kujikwamua kutoka kwenye umasikini.

Mahiza, alisema maaofisa ugani wanatakiwa kusaidia kutoa elimu kwa wakulima ili waweze kulima zao hilo kitaalamu na kupata mbegu bora na kwamba bila hivyo hakuna mafanikio yatakayopatika.

Alisema,chama hicho kimejipanga kupambana na vikwazo vya soko la zao hilo ambapo vikitolewa wakulima watachangia kuinua uchumi wa taifa na kuondoa umasikini wa kaya.

Mahiza,alisema kuwa kwasasa Taccapa kipo katika mpango wa kujenga kiwanda kikubwa cha Muhogo ambacho kitahudumia Mikoa ya Kanda ya Mashariki na Kati na kufanya Muhogo kupata soko kubwa zaidi.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Dkt.Dolphine Magere,alisema kuwa kikao hicho kinalenga kutoa dira ya kuhakikisha zao Muhogo linapata hadhi kama mazao mengine.

Magere,alisema baada ya kikao hicho timu mbalimbali kupitia Halmashauri zitaundwa kwa kuwashirikisha maafisa ugani ili kusudi wawe karibu na wakulima wa zao hilo.

.

 

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.