• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kunenge Aiasa Chalinze Fm kutoa taarifa za maendeleo

Posted on: April 28th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amezihamasisha halmashauri za mkoa huo kuanzisha redio za kijamii ili kuweza kutoa taarifa zitakazosaidia kutatua changamoto katika jamii kwa kuhabarisha, kuburudusha na kutoa elimu juu ya mambo yanayofanywa na Serikali na yale yanayopaswa kuzingatiwa na wananchi pamoja.

Kunenge aliyasema hayo Aprili 29, 2023 alipotembelea na kukagua Kituo cha Redio cha Chalinze FM 97.5 "Sauti ya Jamii" ambacho kimeanzishwa kwa gharama zilizopatikana kupitia mapato ya ndani ya Halmshauri ya Wilaya ya Chalinze.

Kunenge amepongeza jitihada ya Halmashauri hiyo kuweza kuanzisha Mradi huo ambao ni wa kwanza katika mkoa wa Pwani na kuwa kituo hicho kinasikika katika Wilaya yote ya Bagamoyo na maeneo mengine ya jirani kupitia mawimbi ya 97.5 FM.

"Kituo hiki ni kizuri na cha kisasa, Wananchi wanaweza kupata taarifa, kujua juu ya mambo yanayofanywa na serikali pamoja na chama tawala na hasa katika masuala ya kiafya, elimu, utunzaji mazingira, kuboresha maadili kwa vijana na watoto kwani kwa sasa kuna changamoto kubwa ya mmomonyoko wa maadili yanayofanyika," alisema Kunenge.

Aliongeza kuwa kwa kutumia redio hiyo serikali itaweza kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na masuala mbalimbali ya kimaendeleo na akaelekeza kuandaliwa vipindi vyenye maudhui yenye maadili sahihi tofauti na yale yanayopotoshwa na baadhi ya vyombo vya habari na akasisitiza kuwa kwa kutumia kituo hicho wananchi wataweza kusikiliza, kujifunza na kupata taarifa sahihi juu ya mambo yanayozingatia maadili ya nchi ya Tanzania na ya dini za watanzania.

"Tuzingatie kuwa na vipindi vizuri ambavyo vitasaidia kutatua changamoto katika jamii kwa maana ya kuhabarisha serikali inafanya nini na kutoa elimu kuhusu mambo gani wanapaswa kuzingatia, kituo hiki pia kiweze kuburudisha baada ya kazi za kulitumikia taifa, kazi za kijamii na za kiuchumi." aliongeza Kunenge.

Aliongeza kuwa pamoja na mambo hayo, uanzishwaji wa redio hiyo pia utasaidia kutoa ajira kwa vijana na akatoa rai kwa Wafanyabiashara na Wawekezaji Mkoani humo kutumia Kituo hicho kutangaza bidhaa wanazozalisha au huduma wanazotoa.

Katika hatua nyingine, akiwa kituoni hapo, Mhe. Kunenge pia alitoa taarifa kuwa Mkoa wa Pwani unatarajia kuupokea mwenge wa Uhuru Mei 15, 2023 ukitokea Mkoani Morogoro na utakimbizwa katika Wilaya zote saba na hamalashauri tisa kisha utakabidhiwa Mkoani Dar es Salaam Mei 24, 2023, hivyo akawaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika mapokezi hayo na kwenye maeneo yote utakakopitishwa kukagua, kuweka mawe ya msingi au kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mbali na mradi huo, Mhe. Kunenge pia alikagua mradi wa stendi ya magari ya abiria chalinze, pia akafika na kukakagua ujenzi wa mradi wa barabara, nyumba za watumishi wa afya na taa za barabarani katika mji wa Bagamoyo.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.