• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

Kuongezeka kwa shughuli za Kibinadamu zasababisha hatari ya kuharibika kwa Barabara katika kipindi cah Mvua

Posted on: March 10th, 2020

Wakala wa Barabara Mkoani wa Pwani (TANROADS) imesema ongezeko la shughuli za kilimo kandokando ya mito hususani ndani ya mto Rufiji zinachangia kuzuia maji kupita na kukusanya mchanga katikati ya daraja hali ambayo inaweza kusababisha hatari ya kukatika kwa barabara wakati wa mvua.

Hayo yameelezwa katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Pwani kilichofanyika jana mjini Kibaha na kuwahusisha Wakuu wa Wilaya za Mkoa huo, wakurugenzi na wahandisi kutoka TANROADS na TARURA.

Akitoa taarifa ya mpango wa bajeti wa mwaka wa fedha 2020/2021 wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Pwani (TANROADS) bi. Christina Nyamziga ambaye ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Mipango aliainisha changamoto hiyo kuwa imekuwa kikwazo kwa barabara kudumu kwa muda mrefu bila matengenezo.

Bi. Nyamziga alisema mbali ya kilimo pia ipo changamoto ya wizi wa samani za barabara, ongezeko la mifugo kwa baadhi ya maeneo ya Mkoa huo pamoja na upatikanaji wa changarawe inayofaa kwa ujenzi.

"Changamoto nyingine ni kutopatikana kirahisi mtaalam wa matengenezo ya mizani ya Vigwaza inayopima magari yakiwa yanatembea, wakati mwingine ikitokea uharibifu katika mzani magari yote huingia kupima kwenye mzani mmoja hali ambayo husababisha foleni na usumbufu kwa watumiaji wa barabara" alisema.

Bi Nyamziga aliwasilisha taarifa ya mapendekezo ya shilingi milioni 973.820 kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara kutengeneza kilomita 16.40, na shilingi bilioni 1.75 kugharamia miradi ya Serikali Kuu kwa kutengeneza kilomita 25 za barabara za Mkoa.

Alibainisha kuwa kiasi cha shilingi bilioni 4, 94 kimelenga kugharamia miradi ya Serikali Kuu kwa kujenga kilomita 5.7 za barabara kuu.

Nyamziga alisema, katika bajeti ya mwaka 2019/2020, jumla ya shilingi bilioni 22.47 zilipangwa kutumika katika matengenezo mbalimbali ya barabara.

Alisema hadi kufikia mwezi Desemba shilingi bilioni 8.697 zilipokelewa kwa ajili ya matengenezo ya barabara mbalimbali, ambapo Shilingi bilioni 3.424 zimetumika kufanya matengenezo ya barabara kuu na za Mkoa.

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alitoa rai kwa Wakala wa Barabara Mkoa wa Pwani na Wakala wa Barabara Vijijini na Mjini kuhakikisha wanasimamia barabara ziendane na thamani ya fedha zinazotolewa.

Aidha  Amewataka wakala hao  TANROAD na TARURA  Mkoa wa Pwani kushirikiana na viongozi wa Vijiji ,Kata,Tarafa na Wilaya  katika kulinda miundombinu  na kufahamu hali ya Barabara  wanazoudumia katika pindi hiki cha Mvua.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.

  • Situs Toto
  • Situs Slot Gacor
  • AXL777
  • Situs Toto
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • Toto Togel
  • Situs Toto
  • AXL777
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Slot Gacor
  • Toto Slot
  • Toto Slot
  • DORA77
  • KOI200
  • KOI200
  • SILVAWIN
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • YAMITOTO
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200