• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Maafisa Habari Pwani Wqashiriki Warsha ya Mawasiliano ya Kimkakati kupitia Program ya Shule Bora.

Posted on: July 8th, 2025

Maafisa Habari wawili kutoka Mkoa wa Pwani wameshiriki katika warsha ya siku tano ya mafunzo ya mawasiliano ya kimkakati yaliyoandaliwa kupitia Programu ya Shule Bora. Mafunzo hayo yanafanyika katika Ukumbi wa Korogwe Executive, wilayani Korogwe, mkoani Tanga, yakiwa na lengo la kuwajengea washiriki uwezo wa kitaalamu na kiufundi katika nyanja ya mawasiliano ya maendeleo.

Warsha hiyo imefunguliwa rasmi na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Tanga ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uratibu na Mipango Mkoani humo Amina Kibunde, aliyesisitiza umuhimu wa Maafisa Habari wa Serikali na taasisi kuimarisha jitihada za uhamasishaji na utoaji wa taarifa kuhusu miradi ya maendeleo, hasa ile inayotekelezwa katika sekta ya elimu.

“Mafunzo haya yamekusudiwa kuwajengea uwezo wa kiufundi Maafisa Habari katika kuandaa na kusambaza maudhui yanayoonyesha mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya elimu nchini kwani Serikali imefanya mambo makubwa na mazuri hivyo ni jukumu lenu kuhakikisha wananchi wanayafahamu kupitia mawasiliano yenye tija,” alisema Amina.

Ameongeza kuwa kuna haja ya kutumia mifumo mbalimbali ya mawasiliano kueneza taarifa za miradi ya serikali ili kuunga mkono juhudi za maendeleo, huku akiwataka Maafisa Habari kuhakikisha maudhui wanayoyaandaa yana manufaa, yanaongeza uelewa kwa wananchi na kuchochea ushiriki wao katika maendeleo ya taifa.

Kwa upande wake, Kiongozi wa Timu ya Programu ya Shule Bora, Bi. Virginie Briand, alibainisha kuwa warsha hiyo inalenga kusaidia Maafisa Habari kuwasilisha mafanikio ya Programu ya Shule Bora, na kuwawezesha kushiriki katika kuandaa mpango mkakati wa mawasiliano unaolenga kuendeleza mafanikio ya programu hiyo hata baada ya kufikia ukomo wake.

Katika siku ya kwanza ya mafunzo, washiriki walipata nafasi ya kujifunza mada mbalimbali ikiwemo muhtasari wa Programu ya Shule Bora (Shule Bora Overview), misingi ya mawasiliano ya kimkakati, uandaaji wa mikakati ya mawasiliano, na mbinu za kujenga uwezo wa kitaaluma katika kuwasilisha taarifa zenye athari chanya kwa jamii.

Mafunzo hayo yamewakutanisha Maafisa Habari wa Serikali kutoka Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Taasisi za elimu zinazofanya kazi na Shule Bora, pamoja na Maafisa Habari kutoka Mikoa tisa ambayo ni Dodoma, Simiyu, Mara, Singida, Kigoma, Katavi, Rukwa, Tanga na Pwani

Kwa upande wa Mkoa wa Pwani, washiriki wa warsha hiyo ni Zablon Bugingo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, na Hidaya Hadoswa, Afisa Habari Daraja la Pili.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Waziri Mchengerwa aipongeza Shule ya Sekondari ya wavulana Kibaha kwa Ufaulu wa Kiwango cha Juu

    July 10, 2025
  • Mkoa wa Pwani na Program ya Shule Bora waimarisha uelewa wa mabadiliko ya Tabianchi kwa Wataalam wa Halmashauri

    July 09, 2025
  • Pwani yajipanga kumaliza Chanjo na Utambuzi wa Mifugo ndani ya siku 30

    July 09, 2025
  • Maafisa Habari Pwani Wqashiriki Warsha ya Mawasiliano ya Kimkakati kupitia Program ya Shule Bora.

    July 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.