• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Marufuku Kituo kwa cha Afya Pwani Kupata nyota Sifuri-Waziri Jaffo

Posted on: July 10th, 2018

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mh Suleiman S. Jaffo  amemtaka Mganga Mkuu wa Mkoa  wa Pwani  kuhahikikisha kuwa hakuna kituo  cha Afya katika mkoa huo kinachopata nyota sifuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hayo ameyasema wakati wa uzinduzi wa wodi ya wazazi pamoja na jengo la huduma ya dharura katika hospitali ya wilaya ya Bagamoyo, Majengo hayo yamejengwa kwa ufadhili wa taasisi ya Dhinureyin Islamic Foundation iliyoko Mkoani Iringa.

Aidha amesisitiza juu ya utoaji wa huduma bora za Afya katika vituo vyote vya afya Mkoani Pwani na kuongeza kuwa hakuna sababu ya kituo chochote cha Afya nchini kushindwa kutoa huduma bora kwa wananchi.

Katika Hatua nyingine Waziri Jaffo ameipongeza taasisi hiyo ya dini ya Dhi Nureyin kwa kuweza kujenga majengo hayo ya kisasa ambayo ni muhimu katika kutoa huduma ya Afya kwa jamii katika Mkoa wa Pwani.

 Pia amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Alhaj. Majid Hemed Mwanga  kwa kuweza kufuatilia ufadhili na ujenzi huo kwa karibu zaidi hadi kufanikisha kupata majengo hayo.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe.Mhandisi Evarist Ndikilo amesema kuwa kupatikana kwa majengo hayo ni ukombozi kwa wananchi wa wilaya ya Bagamoyo na Mkoa wa Pwani  kwa ujumla kwani kumekuwa na ongezeko la msongamano wa wagonjwa  wanaohitaji huduma ya dharura katika hospitali nyingi za Mkoa wa Pwani.

Mhandisi Ndikilo aliwataka wananchi pamoja na wadau mbalimbali wa Afya nchini  kuiga mfano wa taasisi ya DhiNureyin kwa kushirikiana na Serikali katika kuboresha huduma za Afya.

Aidha Mwenyekiti wa Taasisi ya Dhi Nureyin Sheikh Said Abry amesema kuwa majengo hayo mawili yamegharimu kiasi cha shilingi millioni 703 za Tanzania na amesema   mbali na ujenzi huo pia wamefadhili vifaa tiba vyote vitakavyowekwa ndani ya majengo hayo.

 Sheikh Abry ameongeza kuwa taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali katika kusaidia kuboresha sekta mbalimbali katika maeneo yote Nchini .




Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RAS Pwani asisitiza Ushirikiano Walimu, Wazazi shuleni

    March 06, 2023
  • RC Kunenge atahadharisha Kongani SINOTAN Kutokwamishwa

    March 06, 2023
  • RC Kunenenge aelekeza TEMESA kuwasilisha Mpango matengenezo kivuko Mafia

    March 03, 2023
  • Rais Dkt Samia atengua umiliki Shamba namba 934 Mapinga Bagamoyo

    February 27, 2023
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.