• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Mchatta: Kuna Haja gharama Ujenzi Mafia Kuangaliwa upya

Posted on: May 5th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Rashid Mchata, leo Mei 5, 2023 ametembelea na kukagua ujenzi wa miradi ya maendeleo wilayani Mafia na kueleza kuwa kuna haja ya kuangaliwa upya gharama za ununuzi na usafirishaji vifaa katika wilaya hiyo.

Aliyasema hayo baada ya kubaini kuwa ununuzi wa vifaa na usafirishaji unagharama kubwa kulinganisha na maeneo mengine ya bara hali inayosababisha miradi mingi kuhitaji nyongeza ya pesa za ukamilishaji.

Akiwa Wilayani humo, Mchata ambaye pia ni Skauti Mkuu wa Tanzania alitembelea na kukagua ujenzi wa miradi ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa dharura (EMD) na mahututi (ICU) kwenye hospitali ya wilaya, ujenzi wa shule ya msingi Mrambani (vyumba 11, jengo la utawala, nyumba mbili za watumishi na vyoo matundu 24) na ujenzi wa barabara ya Kichangachui-Hutchery.

Akitoa taarifa ya Mradi wa ujenzi wa jengo la wagonjwa wa dharura (EMD) na mahututi (ICU) kwenye hospitali ya wilaya ya Mafia, Mganga mkuu wa Wilaya hiyo Zuberi Nzige alieleza kuwa umetekelezwa kwa kutoka Serikali kuu za GoT-TCRP (UVIKO 19) na mchango wa halmashauri yote kwa pamoja ikiwa ni zaidi ya sh. Milioni 560.

Pamoja na majengo hayo, halmashauri hiyo imenunua vifaa vya kisasa vyenye viwango vinavyokubalika kimataifa vitakavyotumika kupima na kupata taarifa sahihi na za uhakika ya wagonjwa kisha kutoa tiba sahihi.

Alisema kuwa mradi huo unaolenga kusogeza utoaji huduma za afya na kupunguza vifo visivyo vya lazima kwa wagonjwa wa dharura na mahututi nakupunguza gharama za rufaa umekamilika kwa asilimia 100 na utakuwa na manufaa ya kutoa huduma kwa wagonjwa hao na kuhudumia si chini ya wananchi 66,180.

Mradi mwingine uliyokaguliwa na Mchata ni wa ujenzi wa shule ya msingi Mrambani ambako vimejengwa vyumba 11 vya madarasa, jengo la utawala, nyumba mbili za watumishi ambazo kila moja ina uwezo wa kukaliwa na kaya mbili za watumishi (two in one) na vyoo matundu 24 ambao hadi sasa umegharimu zaidi ya sh. Milioni 400 ambapo majengo mengine yamekamilika isipokuwa la utawala ambalo lipo kwenye hatua ya ghebo na nyumba hizo za waalimu ambazo ziko kwenye hatua ya umaliziaji.

Taarifa ya Mwalimu mkuu wa shule hiyo Saida Kilimo ilieleza kuwa chanzo cha fedha ya utekelezaji mradi huo ni za GPE LANES II, mchango wa wananchi pamoja na halmashauri.

Mwl. Kilimo alisema kuwa ujenzi wa shule hiyo umesaidia kusogeza upatikanaji wa huduma ya elimu msingi kwa wanafunzi waliokuwa mbali na shule za msingi za Kilimahewa na Kigamboni, kuhakikisha kila mtoto anapata huduma ya elimu ya msingi na kuwa wakati wa utekelezaji mradi huo pia umetoa ajira za muda kwa wananchi.

Mchata pia alikagua mradi wa ujenzi wa barabara ya Kichangachui-Hutchery yenye urefu wa kilomita 2.3 kwa kiwango cha lami ambao upo katika hatua za mwisho za ukamilishaji ukiwa umegharimu karibu sh. milioni 900.

Mradi huo ambao upo katika hatua za mwisho unaotekelezwa chini ya TARURA na mkandarasi Gsix Investment Ltd. utarahisisha na kuunganisha huduma za kijamii za usafiri na usafirishaji wa uhakika kwa abiria na mazao ya wakulima, wavuvi na wafanyabiashara baina ya vitongoji mbalimbali vilivyopo ndani na nje ya mji wa Kilindoni.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.