• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Mkenda : Vipaumbele elimu viendane na Dira ya Maendeleo 2025

Posted on: October 16th, 2023

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa  Adolf Mkenda, amewataka watendaji wanaotekeleza program mbalimbali za Elimu ya watu wazima na wale wanaopata elimu nje ya mfumo kuweka vipaumbele vitakavyoendana na dira ya maendeleo ya taifa ya mwaka 2025.

Prof. Mkenda ameyasema hayo octoba 13, 2023 kwenye kilele cha maadhimisho ya Juma la Elimu ya watu wazima ambalo kitaifa limefanyika mkoani Pwani.

Amesema serikali ilianza programu ya watu wazima kwa lengo la kuwasaidia wananchi kupata ujuzi utakaowasaidia kukabiliana na changamoto za maisha na kuendana na mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia.

“Kila mmoja ni shahidi wa mafanikio yanayotokana na program hii ya elimu ya watu wazima ambayo ilianzishwa na Hayati Mwalimu Julius Nyerere akilenga kuwasaidia waliokosa nafasi ya kupata elimu kurudi shule kujiendeleza  na wamefanikiwa kujua kusoma, kuandika na kuhesabu pamoja na uwezo wa kufanya shughuli za ujasiriamali,” amesema Prof. Mkenda.

Amewakumbusha watendaji wanaosimamia program ya elimu ya watu wazima kuhakikisha inapatikana kwenye maeneo yote nchini na vituo vinavyoisimamia vitambulike.

Awali, Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI, anayeshughulikia Elimu, Dk. Charles Msonde amesema serikali imewapa jukumu la kutekeleza sera ya elimu kuanzia ngazi ya elimu Msingi hadi watu wazima.

Amesema katika kutekeleza sera ya elimu, wamebaini changamoto mbalimbali kama vile baadhi ya wanafunzi wanaomaliza darasa la kwanza hadi la nne kutokujua kusoma, kuandika wala kuhesabu.

Ameongeza kuwa kuna changamoto ya umaahiri wa lugha ya kiingereza kwa wanafunzi wa sekondari ambapo matokeo ya mwaka 2022 ya wanafunzi milioni 1.7 waliofaulu kuingia kidato cha kwanza ni asilimia 29 ndio waliofaulu somo hilo huku umahiri wa lugha hiyo ukiwa mdogo kwa asilimia 71 ya wanafunzi wengine.

Amesema baada ya kubaini tatizo hilo, walianzisha utekelezaji wa malengo ya muda mfupi na mrefu kwa kuanzisha program za kuwajengea uwezo wanafunzi hao kujiamini na kuweza kuongea lugha ya kiingereza.

“Baada ya kuanza kutekeleza  mpango huo kuanzia mwezi Januari hadi Septemba mwaka huu, asilimia 96 ya wanafunzi wanaojua kusoma, kuandika na kuhesabu, darasa la pili ni asilimia 99  na wanafunzi wa kidato cha kwanza ndani ya miezi minne hadi mitano wamefundishwa umahiri wa kujua kuandika na kuzungumza kiingereza,” amesema Msonde.

Mkuu wa mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema wanafunzi 1943 wanaendelea na elimu ya watu wazima huku wanakisomo 2080 wakisoma masomo ya uzalishaji mali kama vile ususi, kilimo, utengenezaji wa batiki na shughuli nyingine za mikono ambazo zinawaingizia kipato.

Amesema mpango huo pia umewasaidia vijana kujiunga na vyuo vya ufundi stadi kwa ajili ya kupata ujuzi wa aina mbalimbali na kwamba katika program ya elimu ya masafa kwa mkoa huo, jumla ya wanafunzi 1013 wanaendelea na masomo.

“Licha ya jitihada zinazofanywa na serikali katika kuhakikisha elimu ya watu wazima inakuwa na tija kwa jamii, zipo baadhi ya changamoto katika utekelezaji wa program ikiwamo walimu wa kujitolea kutopata mafunzo ya MEMKWA, wawezeshaji kutolipwa stahiki zao, uhaba wa vitendea kazi kama vile vitabu na miongozo,” ameeleza Kunenge.

Aidha amebainisha mikakati ya mkoa kuwa ni kupunguza idadi ya wasiojua kusoma kuandika na kuhesabu, kuihamasisha jamii kutowatenga watoto wa kike walionufaika na program hiyo wanapohitimu masomo na kurudi nyumbani badala yake wawape ushirikiano ikiwemo kuwatafutia ajira.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.