• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Mkoa Pwani kuuza zao la Ufuta kwa mfumo wa Stakabadhi ghalani

Posted on: May 28th, 2020

Hayo yamebainishwa Mei 27  2020 Kwenye Kikao cha Wadau wa Ufuta Mkoani Pwani.

Akifungua Kikao hicho Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo Mkuu wa Mkoa wa Pwani amesema

"Ufuta ni Uchumi wa Mkoa wetu na Taifa kwa Ujumla hivyo tumekutana kuweka mipango ya kufanikisha mauzo ya Ufuta kupitia mfumo wa Stakabadhi Ghalani katika minada itakayo fanyika katikati ya Mwezi Juni".

Mhandisi Ndikilo ameeleza kuwa Mkoa wa Pwani ni Mkoa unaozalisha zao la Ufuta kwa wingi Nchini. akitolea mfano wa Msimu wa mwaka 2019/2020 amesema jumla ya Tani 7,327 zenye thamani ya shilingi Bilioni 19.35 zilikusanywa na kuuzwa kupitia Maghala ya AMCOS.

Aidha aliendelea kusema kuwa Matarajio kwa Msimu wa Mwaka huu 2020/2021 unatarajiwa kuwa ni Tani 13.25 mara mbili ya mwaka jana.

Pia amesisitiza kuwa ni wajibu wao kama Serikali ya Mkoa kuhakikisha zao hilo linamnufaisha Mkulima. “hawa ni wakulima wanyonge ambao Serikali inataka tuwalinde kwa nguvu zetu zote “alisema Ndikilo.

Akizungumzia Mfumo utakao tumika Mhandisi Ndikilo ameeleza kuwa kwa msimu huu Minada itafanyika kwa njia Kielectroniki kupitia Soko la bidhaa Tanzania (Tanzania Mercantile Exchange- TMX) na kwa njia ya Sanduku. litaanza Sanduku kwa wanunuzi kuweka bei na baadae litafungwa wataendelea na mtandao mwisho watalinganisha bei kupata bei nzuri inayomnufaisha Mkulima.

Akielezea Mfumo huo alisema, Wanachama na wakulima watapeleka ufuta kwenye Maghala ya vyama vya ushirika vya msingi ambavyo vitapeleka ufuta kwenye maghala makuu yaliyosajiliwa na Bodi ya Leseni za Maghala Tanzania, baadaye maghala makuu yatapeleka taarifa za ufuta uliopokelewa TMX ambayo itaratibu minada hiyo .

Katika hatua nyingine alielekeza wakulima walipwe katika akaunti zao na wakala wa vipimo wasimamie ubora wa mizani ili wakulima wasipunjwe .

Hata hivyo ,aliwaelekeza viongozi na watendaji wa vyama vya ushirika wahakikishe vifungashio vya ufuta ghafi vinapatikana kwa wakati kwa wakulima.

Mara baada ya Mnada kufanyika malipo yafanyike haraka kwa Wakulima na wanunuzi wajitahidi kutoa mzigo kwa haraka kwenye maghala ili kutoa nafasi kwa mzigo mwingine unaofuata.

Mhandisi Ndikilo alitoa rai kwa wadau wote wanaohusika kutimiza wajibu wao kikamilifu ili kuwapa manufaa Wakulima kwenye zao la ufuta.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.