• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Mkoa wa Pwani na Program ya Shule Bora waimarisha uelewa wa mabadiliko ya Tabianchi kwa Wataalam wa Halmashauri

Posted on: July 9th, 2025

Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na Programu ya Shule Bora na EdTech umeendesha warsha ya siku moja kwa ajili ya kuwajengea uwezo wataalamu kutoka Sekretarieti ya Mkoa pamoja na Halmashauri za Kibiti na Rufiji, kuhusu mfumo unaopendekezwa wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Warsha hiyo imefanyika katika ukumbi wa Holiday Inn jijini Dar es Salaam, ikiratibiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani kwa lengo la kuongeza uelewa wa wataalamu juu ya matumizi ya taarifa sahihi na mbinu bora za kuelimisha jamii kuhusu athari za mabadiliko ya hali ya hewa na namna ya kukabiliana nazo.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Mwalimu Albert Machua aliishukuru Programu ya Shule Bora na EdTech kwa kufanikisha warsha hiyo muhimu, na kupongeza washiriki kwa ushiriki wao wa kina na michango waliyoitoa katika kujenga mifumo madhubuti ya tahadhari kwa jamii.

“Mafunzo tuliyoyapata yatatusaidia sana katika maeneo yetu kujiandaa na kukabiliana na majanga mbalimbali. Ni muhimu tuendelee kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kutafsiri taarifa hizi, ili waweze kuchukua tahadhari mapema,” alisema Machua.

Aidha, alieleza kuwa matukio ya majanga yanayotokana na mabadiliko ya hali ya hewa yameendelea kujirudia mara kwa mara katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Pwani, hivyo ni muhimu kuchukua hatua za mapema, kwa kuwa hakuna njia ya kuyaepuka bali ni kuyakabili kwa maandalizi ya kitaalamu na ya kijamii.

Kwa upande wake, akizungumza kwa niaba ya Kiongozi wa Programu ya Shule Bora, Ndugu Flavian Lihwa alipongeza juhudi kubwa zinazofanywa na Mkoa wa Pwani katika kukabiliana na majanga yanayoathiri miundombinu ya shule na utoaji wa elimu. Alisisitiza kuwa Programu ya Shule Bora itaendelea kushirikiana kwa karibu na serikali katika kuimarisha mifumo ya kupunguza athari za majanga kwenye sekta ya elimu.

Warsha hiyo ni sehemu ya juhudi endelevu za Mkoa wa Pwani kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya elimu na maendeleo ya jamii katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, kwa kutumia mifumo jumuishi ya taarifa, elimu na teknolojia

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Waziri Mchengerwa aipongeza Shule ya Sekondari ya wavulana Kibaha kwa Ufaulu wa Kiwango cha Juu

    July 10, 2025
  • Mkoa wa Pwani na Program ya Shule Bora waimarisha uelewa wa mabadiliko ya Tabianchi kwa Wataalam wa Halmashauri

    July 09, 2025
  • Pwani yajipanga kumaliza Chanjo na Utambuzi wa Mifugo ndani ya siku 30

    July 09, 2025
  • Maafisa Habari Pwani Wqashiriki Warsha ya Mawasiliano ya Kimkakati kupitia Program ya Shule Bora.

    July 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.