• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

MWENGE WA UHURU WATEMBELEA SHAMBA LA RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA NNE DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE

Posted on: June 9th, 2017

Rais mstaafu wa awamu ya nne  ambae pia ni mkulima wa matunda ya mananasi,Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewataka wamiliki wa viwanda vya matunda kuacha kuwakandamiza wakulima kwa kununua matunda kwa gharama ya chini.

Amesema viwanda hivyo vinasaidia kupatikana kwa masoko ya ndani lakini vimekuwa havina  uwiano wa gharama zinazolingana na maumivu anayoyapata mkulima.

Aidha  Dkt. Kikwete ameeleza kumekuwa na changamoto ya kushuka kwa soko  kwa wakati mwingine hali inayokuwa ikisababisha wakulima kupata hasara kwa matunda kuoza yakiwa mashambani.

Hayo ameeleza wakati akitoa taarifa ya shamba lake la  mananasi lililipo Bago-Kiwangwa  Wilayani Bagamoyo, wakati Mwenge wa Uhuru ulipokwenda kutembelea shamba hilo.

Rais mstaafu Dkt. Kikwete alieleza, viwanda vya usindikaji matunda mbalimbali  vinapaswa kumjali mkulima ambae amekuwa akipata shida na kutumia gharama kubwa kuandaa shamba.

“Wakati utafika watakosa matunda, kutokana na gharama yao hailipi, wakulima wa matunda tushindwa kukubali kuuza kwa bei ya chini ambayo hailipi ” .

Hata hivyo Rais huyo mstaafu alimwambia kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa 2017, Amor Hamad Amor, kuwa mananasi huvunwa baada ya  miezi 18 tangu kupandwa.

“Bei ya mauzo hutegemea wanunuzi na wachuuzi wadogowadogo ambao hununua kwa ukubwa wa nanasi sh 400 hadi 800 linapovunwa kutoka shambani.

Dkt. Kikwete alisema, shamba lake lina ukubwa wa hekari 200 ambapo hekari 64 ndizo zimelimwa na zipo kwenye hatua ya palizi.    

“Mwenge kwa kuangaza shambani kwangu ni ishara ya nuru, basi nitapata neema baadae, nashukuru kwa kuja kutembelea shamba langu  kujionea shughuli ninazofanya baada ya kustaafu” alisema Rais mtaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.

Kiongozi huyo pia alipita kujionea shughuli za ujenzi wa kiwanda cha Sayona kinachomilikiwa na kampuni mama ya MMI Steel, kilichopo kata ya Mboga.

Afisa Uhusiano wa Kampuni za MMI Steel ikiwemo Sayona, Abubakar Mlawa, alimwambia kwamba, kiwanda cha Sayona kimefikia asilimia 70 ya ujenzi na mwezi Novemba mwaka huu kinatarajia kuanza kazi.

Alieleza kuwa kiwanda hicho, kwasasa kimeajiri watu 100 wakiwemo mafundi ujenzi na kitakapoanza kazi kitaajiri watu 800.

Mlawa alisema, mahitaji makubwa ni matunda zaidi ya tani  tisa kwa siku, hasa maembe, nyanya na matunda mengine hivyo wakulima wa matunda wachangamkie fursa hiyo.

Alisema kiwanda cha Sayona ni moja ya uwekezaji mkubwa Mkoani Pwani, na kinalenga kugharimu dola milioni 55 sawa na shilingi bilioni 120 katika ujenzi wake.

Nae kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa, Amor Hamad, alipongeza Serikali kwa kuondoa ushuru wa mazao ya matunda na kuongeza kodi kwa bidhaa zinazotoka nje  ya nchi hali inayoonyesha taifa kutaka kukuza soko la ndani.

Alimpongeza Rais mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Kikwete na kuwataka wakulima wa zao hilo  kuiga mfano wake wa kulima kwa tija .

Amor aliwataka wananchi kujishughulisha kwa kufuata nyayo za waasisi wetu akiwemo Kikwete na Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda .

 “Niipongeze Serikali kwa jitihada hizo kwani inaonyesha Serikali inataka kukuza soko la ndani ya nchi na wakulima kuthaminika  ili kujiletea maendeleo.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.