• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Ndikillo asisitiza kudumisha amani Kibiti kwenye Siro Cup

Posted on: May 20th, 2018

Timu ya soka ya Mgomba ya wilayani Rufiji imetwaa ubingwa wa Siro Super Cup 2018 kwa kuifunga Mjawa ya wilaya ya Kibiti kwa penati 11-10.

Mchezo huo ulichezwa mwishoni mwa wiki hii katika uwanja wa Samora  uliopo Wilayani Kibiti ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe.  Mhandisi Evarist Ndikilo.

Timu hizo hadi zinamaliza muda wa kawaida wa dakika 90 zilishindwa kufungana na kufanya matokeo kuwa 0-0 ndipo zikaingia hatua ya penati  ambapo Mgomba walipata penati zote 11 na Mjawa  waliokuwa wenyeji wakipata penati 10 na kukosa moja.

Kutokana na ushindi huo Mgomba walifanikiwa  kujinyakulia kiasi cha fedha taslim shilingi 1,000,000/=,kombe,seti ya jezi na medali ya dhahabu  huku Mjawa wakijinyakulia kiasi cha shilingi 500,000/= seti ya jezi na medali  fedha na mshindi wa tatu timu ya Mipeko kutoka wilaya ya Mkuranga wakijinyakulia 300,000/=.

Mfungaji bora Dickson Mhilu alijinyakulia mpira huku mwamuzi bora akijinyakulia jezi kwenye mashindano hayo yaliyokuwa na kauli mbiu ya Kibiti salama Jamii salama.

Akifungua Mashindano hayo ,Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo  amepongeza kiwango kizuri kilichoonyeshwa na timu zote mbili  katika mchezo huo  na ametoa rai kwa wadau wa soka kufika vijijini kuvumbua vipaji  vya wanamichezo  badala ya kuangalia mijini pekee.

Katika hatua nyingine Mhandisi Ndikilo amewaasa wakazi wa Kibiti na Rufiji kudumisha  amani  iliyopo  kwa sasa kwani pasingekuwa na amani kwenye maeneo hayo basi hata michezo hiyo isingeweza kufanyika .

 “Mnapofurahia kushiriki katika  michezo hii mkumbuke kuwa furaha yetu itaendelea kudumu kama mtatambua kuwa usalama ndio unaotufanya tuwepo hapa,bila usalama ndugu zangu tusingeweza kuwa hapa leo  tungekuwa kila mmoja  amekaa kwenye eneo lake kwa kuhofia usalama .

Adui yetu mkubwa ni  uhalifu wa aina yoyote, ni matumaini yangu  kuwa hivi sasa kila mmoja wetu anaelewa vya kutosha juu ya  madhara ya uhalifu, ni wajibu wangu kama kiongozi na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama  kuwakumbusha juu ya hatari inayoweza kuwakuta tena endapo hamtachukua hatua madhubuti za kuzuia na kutokomeza  aina zote za uhalifu.Nawaasa kila mmoja katika nafasi  yake kushiriki katika shughuli za ulinzi na usalama kwa kutoa taarifa  za uhalifu kwa vyombo vya ulinzi na usalama”alisema Ndikilo.

Aidha alisema kuwa mashindano hayo yamedumisha upendo na kuondoa tofauti baina ya wakaazi wa Wilaya tatu za Kibiti,Mkuranga na Rufiji kwa kushiriki katika mashindano hayo kwa mshikamano wa hali ya juu.

Mashindano hayo ambayo yalianza mwezi Aprili yaliandaliwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Inspekta Jenerali (IGP) Simon Siro na kushirikisha kata 54 za wilaya hizo za kanda Maalumu ya Mkoa wa Kipolisi wa Rufiji.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.