• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Ndikilo aapisha Wakuu wa Wilaya waili na kutoa Maagizo16

Posted on: August 4th, 2018

 .Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo amewaapisha wakuu wa Wilaya wapya Mhe. Jokate Mwegelo wa wilaya ya kisarawe na Mhe. Zainab Kawawa wa Wilaya ya Bagamoyo na kutoa maagizo 16 ya kutekelezwa na wakuu wa wilaya hizo.

Moja ya maagizo hayo ni pamoja  kuhakikisha kila mkuu wa wilaya anasimamia  ukusanyaji wa mapato na kufikia asilimia zaidi ya 25 ifikapo septemba mwaka huu pamoja na  kuhakikisha   wamiliki wa makampuni wanapatiwa   namba za utambulisho ( TIN) za  biashara zao ndani ya mkoa badala ya kukatiwa Dar es Salaam kama baadhi yao wanavyofanya na  kuunyima mkoa mapato.

Hafla ya kuwaapisha wakuu hao wa wilaya ilifanyika kwenye viwanja vya ofisi ya mkuu  wa mkoa vilivyopo wilayani Kibaha.

Mhandisi Ndikilo alisema kuwa, wakuu wa wilaya wanapaswa kufanyia kazi suala la makusanyo ya mapato  kuhakikisha kuwa mapato ya  halmashauri yanakuwa si chini ya asilimia 25 .

Aidha aliwataka  wakuu hao wa wilaya,kuhakikisha wanadhibiti  na kusimamia vyanzo vya mapato ya ndani ikiwemo mchanga na kokoto ili kujua vinaingiza mapato kwa kiasi gani .

“Kuhusu taarifa ya mkaguzi mkuu wa serikali CAG alisema halmashauri zote za mkoa zimepata hati safi lakini msibweteke simamieni sekta zote ili tuendelee kupata hati safi wakati wote.

Pia alimtaka Mkuu mpya wa wilaya ya Bagamoyo ,kudhibiti magendo kwenye bandari bubu zaidi ya 19 zilizopo Bagamoyo ambazo zinainyima serikali mapato.


Aidha aliwataka waheshimiwa Jokate Mwegelo na Zainab Kawawa  kwenda kuuliza kwenye wilaya zao kama kuna kamati za amani na kama hazipo hakuna waunde kamati hizo mara moja.

“Hakikisheni mnadhibiti migogoro ya ardhi, wakulima na wafugaji kwani kwa mkoa wa Pwani damu iliwahi kumwagika kwenye wilaya za Bagamoyo, Kisarawe, Rufiji na Chalinze alisema mhandisi Ndikilo “


Alisisitiza utunzaji wa hifadhi  za misitu na kuilinda ili isivamiwe na kukabiliana na uharibifu wa mazingira ikiwa ni pamoja na kukata mkaa,kuni na mbao .Katika hilo ,alimuasa Mhe. Jokate na Mhe. Zainabu kwenda kusimamia hifadhi ya misitu mikubwa ya Kazimzumbwi -Kisarawe na Uzigua na Ruvu Kusini na Kaskazini-Bagamoyo.

“Nasisitiza maelewano baina ya viongozi wa ngazi mbalimbali kwani baadhi yao hawaelewani hili ni tatizo ambalo halipaswi kuendelea kwani wanaoumia ni wananchi ambao wanapaswa kuongozwa,” alisema Ndikilo.

Kuhusu sekta ya maji ,alimuagiza mkuu wa wilaya ya Kisarawe Mhe Jokate kumsimamia mkandarasi wa maji kutoka Mloganzila kwenda Kisarawe ili akamilishe kazi kwa wakati  alisema tatizo la maji ni kubwa wilayani humo hivyo ahakikishe anakuwa mstari wa mbele kushirikiana na mkoa kuusukuma mradi huo ukamilike ili kumtua ndoo mama kichwani.

Kwa upande wao wakuu wa Wilaya ya Kisarawe Mhe ,Jokate Mwegelo na Zainab Kawawa  Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo walisema wamepokea maagizo yote na watayafanyia kazi.
Mhe.Jokate alieleza ,hatomuangusha Mhe.Rais, Mkuu wa Mkoa na wananchi wa Kisarawe na kudai hajaenda kutengua torati bali anakwenda kuiimarisha,na kuwaomba wananchi na watendaji wa wilaya yake wote wakutane kazini.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.