Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Ni marufuku kuvamia mashamba pori Pwani : Mhandisi Ndikilo

Posted on: January 8th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Mhandisi Evarist Ndikilo amewataka wananchi waliovamia eneo la Pangani Wilayani Kibaha lenye ukubwa wa hekari 500 na kujigawia viwanja kuondoka mara moja,ili kuiacha Halmashauri kufanya taratibu ya  kurudisha eneo hilo Serikali, baada ya mmiliki wake kushindwa kuliendeleza na kuwa sehemu  ambayo watu wanauawa na kutupwa humo.

Aidha amelitaka jeshi la polisi kumkamata mtu yoyote atakayekutwa kwenye eneo hilo, na kuwataka  wale  wahusika ambao ni matapeli waweze kukamatwa kwa kuwauzia watu kinyume  cha sheria kwani eneo hilo linamilikiwa kihalali.

Mhandisi Ndikilo aliyasema hayo alipotembelea eneo hilo ambalo linamilikiwa na mtu anayefahamika kwa jina la seamens na maeneo mengine yenye ukubwa wa hekari 500 yanayomilikiwa na watu wengine wawili ambao hawajaendeleza kwa muda mrefu, hivyo wananchi kujigawia viwanja wakidai kuwa eneo hilo limekuwa sehemu ya wahalifu kufanya mauaji, au kutupa maiti kutoka maeneo mbalimbali.

Alisema kuwa kuna watu 18 ambao wanajifanya ndiyo viongozi na wamewagwia watu hatua 30 kwa 30 kwa kila mtu katika  eneo hilo ambalo wahalifu wamelifanya eneo hilo kwa ajili ya kupumzika baada ya kufanya uhalifu au wanapowateka watu au kuwaua.

“Kuanzia sasa sitaki kuona mtu katika eneo hili na jeshi la polisi naligiza likamate mtu yoyote watakayemkuta humu, na  achukuliwe hatua kwani ardhi haipatikani kwa njia hizo, kwa sasa acheni Serikali iendelee na taratibu zake za mchakato wa kurudisha eneo hili na mengine ambayo hayajaendelezwa kwa muda mrefu, kwani kwa sasa mamlaka  zinazohusika zinaendelea na urejeshwaji eneo hilo serikalini, kwani liko chini ya mmiliki wake hadi hati ya eneo hilo itakapofutwa”alisema Ndikilo.

Aidha alisema kuwa kwa wale waliouziwa watoe taarifa polisi, ili wahusika waliouza Ardhi wakamatwe, na Mkuu wa Wilaya awasake watu hao ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao, kwakua hawawezi kuuza eneo la mtu ambaye anamiliki kisheria hata kama hajaendeleza kwani  kuna taratibu zake za kumiliki ardhi lakini si kwa njia hiyo.

“Tunajua kuna mahitaji makubwa ya ardhi lakini si kwa utaratibu huu mchakato unaendelea tutapeleka mapendekezo kwa Waziri wa ardhi nyumba na makazi naye atapeleka kwa Rais kwa ajili ya kufuta umiliki, kisha Halmashauri litapanga utaratibu na kuwagawia wananchi kutegemea na mahitaji ya viwanja na mipango miji. mmiliki hatarudishiwa kwani alisema kuwa anataka kukata viwanja ili auze hapana”alisema Ndikilo.

Aliitaka hiyo kamati iliyounda na kuwazuia watu warudishe fedha kwa wale waliowauzia kwani wamewatapeli na Serikali haiwezi kulifumbia macho jambo hilo kwani mara baada ya kurudi litapangiwa utaratibu kwani kwa sasa mji huo unapangwa ili kuelekea kuwa manispaa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha  Assumter Mshama alisema kuwa wananchi hao kutoka maeneo mbalimbali ya Kibaha na Dar es Salaam waligawana  maeneo hayo ambayo yanamilikiwa na watu watatu.

Mshama alisema kuwa mmiliki wa kwanza eneo lake lina ukubwa wa hekari 300,mwingine hekari 200 na mwingine hekari 500. ambapo wananchi waliamua kugawana viwanja kinyume cha sheria wakidai kuwa eneo hilo limekuwa likitumika kwa vitendo vya kihalifu.

“Walisema wameamua kugawana eneo hilo wakidai  kuwa wamiliki wameshindwa kuendeleza na kufanya baadhi ya watu wakiuwawa humo hasa waendesha pikipiki au maiti kutupwa kwenye eneo hilo ambalo halijaendelezwa na kuwa msitu”alisema Mshama.

Alisema kuwa baada ya kutokea uvamizi huo wamiliki walifika Ofisi ya Mkurugenzi na kutakiwa kujieleza ni kwa nini wameshindwa kuyaendeleza na kuwataka watoe mpango wa maeneo yao ambapo wengine walitaka kukata viwanja na kuviuza jambo ambalo walikataliwa kwani wameshindwa kuyaendeleza kwa muda mrefu hivyo mchakato wa kuyarudisha Serikalini umeanza.

Naye mmbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini silvestry Koka alisema kuwa eneo hilo lina  wamiliki hivyo ni vema kukaa nao na kuona watawekaje mipango miji ikoje ya Serikali katika kuupanga mji wa Kibaha.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.