• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Pwani Kunufaika na Vyandarua Milioni 1.2 Kukabili Malaria.

Posted on: September 9th, 2025

Mkoa wa Pwani umejipanga kuimarisha mapambano dhidi ya malaria kwa kusambaza vyandarua milioni 1.2 vyenye thamani ya shilingi bilioni 24.

Hatua hiyo inalenga kufikia kaya 454,593 zenye zaidi ya wananchi milioni 2.2 katika wilaya saba na halmashauri tisa za mkoa huo.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, akizungumza Septemba 9, 2025 wakati wa uzinduzi wa usambazaji na ugawaji wa vyandarua hivyo, alisema shughuli hiyo inatekelezwa na Bohari ya Dawa (MSD) kwa mwongozo wa serikali.

"Lengo kuu ni kulinda afya za wananchi hususan watoto, wajawazito na familia kwa ujumla," alisema huku akihimiza wananchi kutumia vyandarua kwa malengo yaliyokusudiwa badala ya kuvigeuza kwa matumizi mengine.

Aliongeza kuwa kila kaya inapaswa pia kuchukua tahadhari zingine ikiwa ni pakoja na kuondoa mazalia ya mbu na kutumia dawa za kunyunyizia, ambazo kwa sasa huzalishwa katika kiwanda kilichopo Mjini Kibaha.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji wa MSD, Victor Sungusia, alisema Mkoa wa Pwani ni wa tatu kunufaika na mpango huo kitaifa baada ya Shinyanga na Kigoma na akabainisha kuwa magari 30 yametengwa kwa ajili ya zoezi hilo na watatumia siku 21 kukamilisha usambazaji na kuwa MSD imekwishasambaza zaidi ya vyandarua milioni 40 tangu kuanza kwa mpango huo.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Dkt. Kusirye Ukio, alifafanua kuwa kwa kipindi cha mwezi mmoja na nusu, timu za afya zilitembelea kata 111 na vijiji 553 na kubaini kaya 454,593 sawa na asilimia 110 ya lengo zitakazopokea vyandarua hivyo.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Pwani Yatenga Maeneo 27 ya Kongani Kukuza Uwekezaji na Viwanda.

    September 11, 2025
  • Lishe Bora Chachu ya Maendeleo - RC Pwani.

    September 09, 2025
  • Pwani Kunufaika na Vyandarua Milioni 1.2 Kukabili Malaria.

    September 09, 2025
  • Timu ya Michezo ya Watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani yashiriki Uzinduzi wa Mashindano ya 39 ya SHIMIWI.

    September 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.