• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Pwani sasa yajidhatiti katika kilimo cha Pamba

Posted on: May 25th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo amewapongeza wakulima wa Zao la Pamba wa Halmashauri ya Chalinze  kwa  kulima zao la pamba kwa wingi  ambapo zao hilo linaonyesha kustawi sana Mkoani Pwani.

Pongezi hizo amezitoa  alipofanya Ziara yake ya kuhamasisha kilimo cha pamba  katikaHalmashauri ya Chalinze na kuvitembelea  Vijiji vya kata ya Mbwewe,Mandera na Miono, ambapo Mhandisi Ndikilo aliweza  kuona  shamba la mfano la  zao la Pamba katika Kijiji cha Kwamkonje na kuona jinsi zao hili inavyostawi katika Halmashauri  ya Chalinze.

Katika kuhamasisha zao hilo   Mhandisi Ndikilo amewataka Wananchi wa Chalinze na Mkoa Pwani kwa ujumla kupambana na hali ya umaskini kwa kulima mazao ya biashara ikiwemo Pamba na Korosho kwani mazao haya yanastawi vizuri katika Mkoa wa Pwani.

“Napenda kutoa rai kwa wananchi wa mkoa Pwani hasa wananchi wa Chalinze na Rufiji tumieni fursa hii ya kulima Pamba kwani Mkoa wetu una ardhi nzuri yenye rutuba inayafaa kwa kilimo cha pamba na korosho ,kwani mazao haya ni mazao ya biashara ambayo yatatusaidia kuondokana na umaskini”alisema Ndikilo.

Katika Hatua nyingine Ndikilo aliwataka wakulima wa zao la Pamba kuzingatia masharti na kanuni za kilimo bora katika uzalishaji ili kujenga thamani na kutoliharibu zao la pamba kwa kuchanganya na mchanga au maji kwani kufanya hivyo hupelekea kuua   soko la zao hilo .

“Napenda kuwaasa wananchi kuwa tuache kuhujumu zao la pamba kwani tutajiharibia soko na tutakuta tunarudi kule kwenye umaskini ,hivyo yeyote atakaebainika kuwa anahujumu zao la Pamba basi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake”alisema Ndikilo

Aidha Ndikilo alimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze kwa kuweka mipango ya kununua pikipiki  kwa ajili ya Maafisa Ugani na kuwataka maafisa hao   kuweza kuwafikia wakulima na kuwasaidia kutumia mbinu bora za kilimo ili kuliongeza thamani zao la Pamba.

“Nimefarijika na taarifa ya Mkurugenzi  wa Halmashauri  ya Chalinze lakini pia kauli ya Mwenyekiti wa Halmashauri  kwamba zao la Pamba linakubalika na pia nimejionea  mwenyewe” Mhandisi Ndikilo alisema.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliweza pia kukagua kiwanda cha kuchambulia pamba kilichopo Kijiji cha Mandera  ambacho kwa sasa hakifanyi kazi, na aliahidi kuwa atafanya kila awezalo  ili aweze kufufua kiwanda hicho.

Mhandisi Ndikilo pia  alitembelea msitu wa Uzigua  kwa lengo la kuona maendeleo ya msitu huo ambapo alishuhudia uoto wa asili  umeanza kurudi, na hali ya msitu imeanza kurejea katika hali yake, na wanyama wameanza kuonekana  ingawa alielezwa kuwa bado ipo changamoto ya wafugaji kuingiza mifugo yao kinyemelea. Ndikilo aliagiza kuwa, zoezi  la kuwaondoa wafugaji  liwe endelevu kwa maslahi mapana ya msitu huo, ambao ni mapito ya wanyama wanaotoka Mbuga ya  Sadan kwenda Wamimbiki.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.