• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Pwani yapendekeza matumizi ya Sh. Bil. 178.025 kuboresha Barabara

Posted on: March 21st, 2019

Mkoa wa Pwani umepanga kutumia kiasi cha shilingi Bilioni 178,024.699 zikiwa ni sh. Bilioni 32.36 za matengenezo na sh. Bilioni 145.662 za maendeleo ili kuboresha miundombinu ya barabara katika mwaka wa fedha 2019/20.  

Taarifa ya hiyo ilitolewa na Wakala wa Barabara Kuu na za Mkoa (TANROADS) pamoja na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kwenye kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa kilichofanyika machi 21, 2019. Kiasi hicho cha fedha kinajumuisha sh. Bilioni 94.671 za TANROADS na sh. Bilioni 83.353 za TARURA ambazo zitatumika katika matengenezo ya kawaida, matengenezo maalum, sehemu korofi, madaraja, kalavati na mifereji.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Pwani ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Kibaha  Mhe. Assumpter Mshama akifungua kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa cha kupitia Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa fedha 2019/20 kilichofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Kibaha Machi 21, 2019.

Katika ufafanuzi wake, Meneja TANROADS Mkoa wa Pwani Mhandisi Yudas Msangi alibainisha kuwa taasisi yake itaboresha barabara zenye urefu wa kilomita 1,009.70 kati ya mtandao wa barabara zenye urefu wa kilomita 1387.98.

Katika mtandao huo, Barabara kuu zina urefu wa kilomita 501.70 na zote ni za lami huku Barabara za Mkoa zikiwa na jumla ya urefu wa kilomita 886.28 (Tabaka la lami ni kilomita 34.13 na za changarawe zikiwa na urefu wa kilomita 852.15.)

Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Bibi. Theresia Mmbando (aliesimama) akitoa maelezo ya awali katika kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa cha kupitia Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2019/20. kilichofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mjini Kibaha Machi 21.

Kwa upande wake mratibu wa TARURA Mkoa Mhandisi Lutufyo Mwakigonja alibainisha kuwa taasisi yake inahudumia mtandao wa Barabara wenye urefu wa jumla ya kilomita 3833.05, kati ya hizo, barabara za lami ni kilomita 37.17, barabara za changarawe ni kilomita 407.92 na barabara za udongo zina na urefu wa kilomita 3,387.96.

Awali, katika hotuba ya ufunguzi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Barabara Mkoa wa Pwani Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo iliyowasilishwa kwa niaba yake na Kaimu Mkuu wa Mkoa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe. Assumpter Mshama aliwakumbusha wajumbe wa bodi hiyo kuwa moja ya majukumu yao kulingana na sheria ya Barabara namba 13 ya mwaka 2007 ni kupokea mipango ya ujenzi na matengenezo ya mwaka ya barabara na kuipitisha kwa lengo la kuhakikisha kwamba maeneo mbalimbali katika Mkoa yanafikika vizuri.

“Mipango na bajeti inayopitishwa visimamiwe na kutekelezwa kwa weledi na uadilifu mkubwa ili matokeo yake yaweze kuwa yenye tija kwetu sisi na kwa jamii nzima ya watanzania kwa ujumla ikizingatiwa kuwa fedha hizo ni za walipa kodi na sisi ndiyo tuliyopewa dhamana ya kuzisimamia” aliongezea Eng. Ndikilo.

Kwa pamoja kikao hicho kilipitisha mpango na bajeti hiyo.

Picha tatu za juu ni baadhi ya wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Pwani wakipitia taarifa za Mpango na Bajeti za Wakala wa Barabara Kuu na za Mkoa (TANROADS) na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kilichofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mjini Kibaha Machi 21, 2019.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani Ndg. Ramadhani Maneno (aliesimama) akichangia hoja kwenye kikao cha kupitia na kujadili Mipango na Bajeti za TANROADS na TARURA kwa mwaka wa fedha  2019/20 kilichofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mjini Kibaha Machi 21,2019.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.