• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

PWANI YAZIDI KUNG'ARA KATIKA UWEKEZAJI - MAKAMPUNI 30 YA CHINA YAONESHA NIA YA KUWEKEZA MKOANI PWANI .

Posted on: November 4th, 2017

Makampuni 30 kutoka nchini China yameonesha nia ya kuja Mkoa wa Pwani - Tanzania , kwa ajili ya kuwekeza kwenye sekta ya mbalimbali za kiuchumi. Ujio wa makampuni hayo ni matunda ya safari  ya timu ya baadhi ya viongozi na wataalam wa Mkoa wa Pwani waliokwenda nchini China hivi karibuni kujifunza masuala mbalimbali ya uwekezaji pamoja na kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo Mkoani Pwani.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo alieleza kuwa, kupatikana kwa wawekezaji hao kuja Mkoani Pwani ni mwendelezo wa uwekezaji mkubwa uliowekwa Mkoani Pwani na makampuni mengi kutoka nchi ya China.

Mhandisi Ndikilo alibainisha kuwa, viongozi na wataalam hao wa ngazi ya Mkoa na Halmashauri ya Kibaha wakiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa Ndg. Zuberi Samataba walitembelea nchini China kuona shughuli zinazofanywa na makampuni mbalimbali.  “Timu hiyo ikiwa nchini China ilitembelea majimbo ya Jiangsu, Anhui, Guangdong na Majiji ya Shanghai na Beijing, waliweza kuona shughuli zinazofanywa na wawekezaji na kushiriki kongamano la wawekezaji na wafanyabiashara lillofanyika Beijing,” alisema Mhe.Ndikilo.

Mhe. Ndikilo pia ameziagiza Halmashuri zote za Mkoa wa Pwani  kuendelea kutenga maeneo maalum  kwa ajili uwekezaji na ujenzi wa viwanda  ili kutekeleza kwa upesi agizo la Serikali la ujenzi wa viwanda mia moja kwa kila Mkoa. Amezitaka Halmashuri hizo wakati zinapotenga maeneo maalum ya uwekezaji lazima zishirikishe kikamilifu taasisi wezeshi kuweka miundombinu muhimu ya maji, umeme pamoja na barabara ili maeneo yaweze kuwavutia wawekezaji kutoka ndani  na nje ya nchi.

Mbali na kutenga maeneo maalum ya uwekezaji  pia amezitaka Halmashuri pamoja na Watendaji wa Vijiji kuendelea kuwakumbusha na kuwaandaa wananchi kuchangamkia fursa za uwekezaji wa viwanda kama kujipatia ajira ili kujikwamua kiuchumi.

Awali akiwasilisha ripoti hiyo Katibu Tawala Msaidizi - Uchumi na Uzalishaji Bw. Shangwe Twamala alisema pamoja na fursa nzuri za uwekezaji zinazotangazwa nchini, zipo changamoto mbalimbali ambazo zinapelekea kuchelewesha mchakato wa uwekezaji. Aidha aliongezea  kuwa ujumbe wa Pwani ulitembelea majimbo matano na kukutana na wafanyabiashara kutoka kampuni 108 za China na kueleza fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo Mkoani Pwani ambapo tayari kampuni 30 kati ya 108 zimeshaonesha nia ya kuwekeza.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.